Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina swali moja la nyongeza; kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, yupo tayari baada ya Bunge hili kwenda kukitembelea kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kwamba niko tayari ratiba itakavyoruhusu tutatembelea eneo hilo ili kuona kiwango cha uchakavu hicho kilichofikiwa.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii kuuliza swali la nyongeza. Ningependa nimuulize Mheshimiwa Waziri, nimekuwa nikisimama mara nyingi kuhusu matatizo ya vituo vyangu vya Chumbuni. Je, sasa nataka kauli yake, yuko tayari kuongozana na mimi mpaka kwenye jimbo langu kutokana na uhalifu umekuwa ukiongezeka na zaidi ya mara sita nimekuwa nikiuliza bila kupata majibu sahihi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pondeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishasema, tutakapokuwa tunakwenda kwa Mheshimiwa Amour kwa sababu kote ni Zanzibar niko tayari pia kupita kwenye jimbo lake ili kuona kiwango cha uhalifu anachozungumza.

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 3

MHE. JANET E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kufuatia changamoto ya Mkoa wa Dar es Salaam maeneo mengi kukosa vituo vidogo vya polisi hususan kata ya Makongo ambayo Serikali ilishaahidi kukamilisha ujenzi huo. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janet kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali kwa nyakati tofauti ilishasema iko tayari kushirikiana na mamlaka za Serikali za Mitaa na Waheshimiwa Wabunge kukamilisha vituo vya polisi vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi. Sasa kupitia Bunge lako tukufu nimuombe Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, labda niseme IGP, kubaini vituo vyote vya Dar es Salaam ambavyo viko njiani havijakamilika kufanya tathmini ya kiwango cha ukamilifu unaohitajika ili viweze kutengewa fedha za kukamilisha vituo hivyo.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 4

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza, Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibondo hakina hadhi ya kituo cha wilaya maana ni kidogo sana lakini pia ni chakavu mno. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo hicho ili kiwe na hadhi ya wilaya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunafahamu kituo cha Kibondo ni kidogo kwa size lakini pia ni chakavu kinahitaji kufanyiwa ukarabati. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kupitia Jeshi la Polisi mpango wa kukarabati kituo hicho kimewekwa katika Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2023/2024 kwa hiyo ukae kwa subira kwamba mwaka ujao tukipitisha bajeti hapa kituo hicho pia kitakuwa kimezingatiwa.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 5

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi Kengeja ambacho kipo Mkoani Pemba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kituo hiki cha Kengeja kipo isipokuwa ni chakavu sana. Nimekitembelea katika ziara yangu ya mwezi uliopita nikajiridhisha kwamba ni kituo chakavu na Wizara kupitia Jeshi la Polisi imekiweka kwenye mpango wa ukarabati katika bajeti ya mwaka 2023/2024.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 6

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Jengo la Polisi Mkoa wa Manyara kwa kuwa takribani ni miaka 10 sasa lipo katika hatua ya msingi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum Manyara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli nasi tumebaini kwamba jengo hilo limekaa muda mrefu na lilikuwa halijapangiwa bajeti lakini nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika bajeti ya mwaka 2023/2024, Jeshi la Polisi limeweka kituo hicho katika mpango wake wa ujenzi.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 7

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante, Kituo cha Polisi cha Mlimba ni kituo ambacho kinatumia majengo ya Shirika la Reli (TAZARA) na majengo yenyewe ni chakavu. Nini sasa mpango wa Wizara kujenga kituo cha polisi pale Mlimba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri swali hili tumelijibu jana lilikuwa limeulizwa na Mbunge mwingine anayetoka Ifakara. Tunatambua uchakavu wa kituo hicho, ahadi ya Serikali ni kwamba kadiri tutakavyopata fedha katika bajeti ya mwaka 2024/2025, vituo hivi tena viwili, Ifakara na Mlimba vitawekwa kwenye mpango wa ujenzi.