Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 46 2023-02-02

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha jengo la Kituo cha Polisi Konde, Wilaya ya Micheweni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk Mbunge wa Tumbe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uchakavu wa jengo la Kituo cha Polisi cha Konde kilichopo Wilaya ya Micheweni. Tathmini ya uchakavu ili kufanya ukarabati imefanyika mwezi Novemba, 2022 na kiasi cha fedha shilingi 92,000,000 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati huo. Fedha hizo zitatengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024.