Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama ya gesi ili kuepuka matumizi ya mkaa na kuni?

Supplementary Question 1

MHE. NORAH W. MZERU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina swali langu la nyongeza, Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Watanzania wa hali ya chini wanapata elimu ya madhara ya kutumia nishati chafu ya kupikia na kuona umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya Wizara ya Nishati ya Mwaka huu wa Fedha, tulieleza moja ya kipaumbele kikubwa ni kuhakiksha kwamba nishati safi na salama ya kupikia inawafikia Watanzania walio wengi. Katika jitihada hizo, elimu kwa Watanzania kuhusu madhara ya nishati chafu ni jambo la muhimu. Itakumbukwa kwamba tarehe 01 Novemba mwaka uliopita Mheshimiwa Rais alizindua mjadala wa Kitaifa wa nishati safi ya kupikia na alitoa maelekezo mahusus ikiwemo ya mjadala ule kuendelea katika maeneo mbali mbali ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, hivi tunavyozungumza, Serikali inaandaa dira ya kuelekea katika nishati safi ya kupikia, dira ambayo itajumuisha elimu kwa umma, elimu ambayo itawafikia Watanzania wote kila mahali walipo. Kwa hiyo, tutazindua dira hiyo mwezi Juni.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama ya gesi ili kuepuka matumizi ya mkaa na kuni?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa gharama kubwa huongezeka kutokana kwamba waagizaji wa gesi hufanya binafsi binafsi, kwa maana hakuna bulk procurement: Je, ni mpango gani wa muda mfupi kuhakikisha bulk procurement inaanza kufanya kazi ili kupunguza na kudhibiti gharama ya gesi inayopanda holela? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama nilivyozungumza kwenye jibu la msingi, uagizaji mkubwa na uwezo mkubwa wa kuhifadhi na miundombinu ya kupakua na kuhifadhi gesi kwa wingi inasaidia kushusha gharama. Ndiyo maana Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imeingia makubaliano ya kuongeza uwezo wa Bandari ya Dar es Salaam kushusha, kupokea na kuhifadhi gesi kwa wingi. Kwa hiyo, Serikali iko mbioni kutekeleza mpango huo.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama ya gesi ili kuepuka matumizi ya mkaa na kuni?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Kwa kuwa kwa kupunguza bei na matumizi ya mkaa mpango mmojawapo ni kutumia gesi asilia: Je, mna mkakati gani wa kuwaingizia majumbani gesi asilia wananchi wa Mkoa wa Morogoro? Ahsante sana.

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, gesi asilia inatoka Mtwara mpaka Dar es Salaam kwa bomba na uwekezaji ule ni wa gharama kubwa kutona na gharama kubwa za ujenzi wa miundombinu ya bomba. Tunaamini kwamba kwa wakati huu mfupi wa sasa, miundombinu ya kujenga bomba la gesi asilia kutoka Dar es Salaam - Morogoro mpaka Dodoma ni mpango wa muda mrefu. Imani yetu ni kwamba tutashirikiana na sekta binafsi kujenga vituo vidogo, vinaitwa ‘vituo dada’ ambavyo vitachukua gesi iliyogandamizwa kutoka Dar es Salaam na kuisambaza katika vituo mbali mbali nchini na baada ya hapo itasambazwa kutokea katika vituo hivyo.

Mheshimiwa Spika, tumeshapokea mpango wa uwekezaji wa jambo hilo na tutautangaza pale tutakapokuwa tumefikia makubaliano na sekta binafsi ya kupeleka gesi hii katika maeneo ambayo ni mbali na Dar es Salaam ambapo bomba halijafika.