Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 43 2023-02-02

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama ya gesi ili kuepuka matumizi ya mkaa na kuni?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tanzania hatuzalishi gesi iliyosindikwa kiwandani (LPG) ambayo pia hutumika kama nishati ya kupikia. Gesi ya LPG huagizwa kutoka nchi za nje. Kama ilivyo kwa bidhaa nyingine zinazotokana na mafuta ya petroli, gharama za LPG pia hutegemea bei katika soko la dunia.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha na kushirikiana na sekta binafsi kuwekeza katika miundombinu ya kupokea na kuhifadhi LPG ili kuwa na uwezo mkubwa zaidi ya tani 16,000 za sasa. Hii itatuwezesha kuanza kuagiza LPG kwa mfumo wa uagizaji wa pamoja na hivyo kupungua kwa gharama za uagizaji na kupata nafuu katika gharama ya gesi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia TPDC imetenga fedha Shilingi bilioni 10 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia ambayo ipo hapa nchini na kuwaunganisha wateja kwa maeneo yaliyopitiwa na mradi wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo kupikia. Gesi hiyo inayotumika kwa kupikia ni nafuu kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na vyanzo vingine vyanzo vingine vya nishati ya kupikia. (Makofi)