Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakasimu kwa TANROADS Barabara ya Kibaoni, Kakunyu hadi Bugango wakati taratibu za kupandisha hadhi zikiendelea?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini pia niendelee kuipongeza Serikali kwa fedha walizotuletea tulizipokea na barabara inaendelea kujengwa.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali imeshasema kwamba itaendelea kuihudumia barabara hiyo mpaka itakapopandishwa hadhi, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni hatua gani imefikiwa ya barabara hiyo kupandishwa hadhi kutoka TARURA kwenda TANROADS kwa sababu ina vigezo vyote vinavyostahili?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, ni nini mkakati wa Serikali kwa barabara za namna hiyo ambazo zina vigezo na zinaunganisha Nchi ya Tanzania na nchi za jirani ili ziweze kuwekwa katika mkakati wa kuzipandisha hadhi kutoka TARURA kwenda TANROADS? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Jimbo la Nkenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara zikishatoka katika ngazi ya TARURA ili zipandishwe hadhi zinakwenda Wizara ya Ujenzi ambao ndio wasimamizi wa TANROADS. Kwa hiyo, hatua ya sasa zipo huko ambapo wanafanya uchambuzi wa mwisho, wakishamaliza nafikiri watatangaza kwenye Gazeti la Serikali kwa taratibu ambazo zimewekwa.

Mheshimiwa Spika, la pili, mkakati wa Serikali ni kuhakiksha barabara hizo kwanza kwa sasa zinapitika wakati wote na kulingana na mahitaji ya wakati uliopo na wakati ujao, maana yake tutaendelea kuzingatia ili kama zinahitaji kupandishwa hadhi zitafanyika hivyo, kama haitahitajika basi tutaendelea kuzihudumia ili zipitike wakati wote, ahsante sana.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakasimu kwa TANROADS Barabara ya Kibaoni, Kakunyu hadi Bugango wakati taratibu za kupandisha hadhi zikiendelea?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Ni lini Serikali itahamisha barabara ya Bashnet – Bassodesh – Hirbadaw - Singida kutoka TARURA kwenda TANROADS kwa kuwa upande wa kutoka Bassodesh - Hirbadaw ipo TANROADS na Singida ipo TANROADS matengenezo yake huwa yako tofauti?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Xaday Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nizielekeze tu halmashauri zenye mahitaji hayo zifuate taratibu na utaratibu unaeleweka unaanzia ngazi za halmashauri baadaye zinaenda katika Bodi ya Barabara Mkoa halafu zinapelekwa Wizara ya Ujenzi kwa ajili ya uthibitisho. Kwa hiyo sisi tunapokea tu kama ombi ili hizo taratibu ziweze kufuatwa, ahsante sana.