Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 38 2023-02-02

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakasimu kwa TANROADS Barabara ya Kibaoni, Kakunyu hadi Bugango wakati taratibu za kupandisha hadhi zikiendelea?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Jimbo la Nkenge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kibaoni, Kakunyu hadi Bugango ina sehemu mbili ambazo zinahudumiwa na Wakala mbili za barabara ambazo ni TANROADS na TARURA. Sehemu ya kwanza ya barabara hiyo inaanzia Kibaoni hadi Kakunyu yenye urefu wa kilomita 76 ambayo inahudumiwa na TANROADS na sehemu ya pili inaanzia Kakunyu hadi Bugango yenye urefu wa kilomita 12.4 ambayo inahudumiwa na TARURA.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa mwaka 2022/2023 kupitia TARURA imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 200 kwa ajili ya matengezo ya barabara kutoka Kakunyu hadi Bugango yenye urefu wa kilomita 12.4 kwa kiwango cha changarawe.

Aidha, Serikali itaendelea kuhudumia barabara hiyo na kuhakikisha inapitika wakati wote hadi hapo taratibu za kupandishwa hadhi zitakapokamilika.