Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali kwa sababu imekuwa ni kilio cha muda mrefu kupata stendi ya kisasa katika Mji wetu Ikungi. Sasa. ili kujiridhisha, ni hatua gani sasa zimeanza kuchukuliwa katika kuanza ujenzi huu mapema?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa fedha zilizotengwa, kwa maana milioni 110, ni fedha kidogo. Nini mkakati wa kuongeza fedha za kujenga stendi yenye hadhi ili tuweze kuwa na stendi kubwa kwa sababu ni main road na inapokea magari mengi yanayoelekea Dar es Salaam na Mwanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna uhitaji wa stendi katika eneo hilo la Ikungi, na tayari shughuli za awali za ujenzi ikiwemo kusafisha eneo lakini pia kufanya upembuzi imeshaanza kwa ajili ya kuanza ujenzi huo; na tunaamini shilingi milioni 110 itaanza kazi katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, lakini tathmini iliyofanyika inahitaji shilingi milioni 700 ili kukamilisha stendi hii ya Ikungi. Tumeshakubaliana kama Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri kila mwaka watatenga shilingi milioni 150 na katika mwaka ujao wa fedha 2023/2024 halmashauri imakwishatenga fedha hiyo kwa ajili ya kuendelea na ujenzi ahsante.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Supplementary Question 2

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais mwaka jana alipotembelea Mji wa Lamadi aliahidi ujenzi wa stendi. Je, ni lini ujenzi huu sasa utaanza ili kuokoa maisha ya watu kwa sababu ya msongamano mkubwa ulioko pale?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe Lusongekile, Mbunge wa Jimbo la Busega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Rais Daktari Samia Suluhu Hassan alielekeza mamlaka za Halmashauri ya Busega kuanza mpango wa kujenga stendi katika eneo la Lamadi. Ofisi ya Rais TAMISEMI tumekwishamwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Busega kufanya tathmini na kuandaa makadirio ya gharama kwa ajili ya kuanza ujenzi huo. Kazi hiyo inaendelea watawasilisha Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya hatua zaidi, ahsante.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongea.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu Mkoa wa Songwe ni Mkoa Mchanga na una uhitaji wa stendi kuu ya mkoa. Serikali imefikia hatua gani katika kuhakikisha ujenzi wa stendi hii unakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwishatoa maelekezo na utaratibu wa mikoa yote na halmashauri zote ambazo zina uhitaji wa miundombinu ya stendi kuandaa maandiko pamoja na kufanya tathmini ili kuziwasilisha Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya kuwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango ili kuona kama inakidhi vigezo vya kuwa miradi ya kimkakati yatafutiwe fedha lakini kama hayakidhi basi kupitia vyanzo vingine vituo hivyo viweze kujengwa. Kwa hiyo naomba nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inalifanyia kazi suala la stendi ya Mkoa wa Songwe na utekelezaji utafanyika, ahsante.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Supplementary Question 4

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ile stendi ya Musoma Mjini Manispaa kipindi kama hiki cha mvua huwa inabadilika badala kuwa stendi inakuwa sawasawa na zizi, kwa maana tope zinajaa. Kwa kuwa Serikali ilishaahidi kuijenga tangu mwaka 2020 ni lini hiyo stendi itajengwa ili na sisi watu wa Musoma tuweze kuwa na stendi nzuri?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vedastus Manyinyi, Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba stendi ya Manispaa ya Musoma ni mbovu na Serikali imeshachukua hatua kwanza kwa kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Musoma kuandaa tathmini ya mahitaji ya gharama za ujenzi, lakini pia kuanza kutenga fdha kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwakumbusha Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini kwamba kunapohitajika miundombinu muhimu kama hii lazima wafanye tathmini, waanze kutenga fedha za mapato ya ndani asilimia 40 au 60 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miradi kama hii ili kuondoa changamoto kwa wananchi, ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Supplementary Question 5

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Mradi wa Miji 45 utakaoboresha miji 45 maarufu kwa jina la TACTIC, sehemu mojawapo ni pamoja na ujenzi wa barabara, lakini pia pamoja na ujenzi wa stendi ambazo zitakuwa chanzo cha mapato cha Halmashauri zetu likiwemo pia Jiji la Mbeya. Je, ni lini mradi huo utaanza ili kuwezesha Halmashauri na Miji hiyo kuwa na stendi za uhakika ambazo zitakuwa pia chanzo cha mapato?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Miradi ya TACTIC imegawanywa katika phases tatu. Tier one, two and three, lakini tier one hatua zinaendelea, tier two na three pia hatua zinaendelea ili kuhakikisha katika kipindi hicho miradi yote hii inatekelezwa kwa kuboresha barabara, masoko lakini pia na stendi katika miji hiyo 45. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mafinga pia itatekelezewa mradi huo kama ilivyopangwa kwenye mpango wa TACTIC, ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Supplementary Question 6

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Stendi iliyopo katika Wilaya ya Karatu haikidhi vigezo na hasa wakati wa masika inakuwa na changamoto kubwa. Je ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa tukizingatia karatu ni mji mdogo wa kitalii?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uhitaji wa stendi katika Halmashauri ya Karatu ni muhimu na ni kweli kwamba kuna uhitaji huo, lakini tumekwishamwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu kufanya tathmini ya gharama, lakini kama gharama ni kubwa juu ya uwezo wa halmashauri, walete kama mradi wa kimkakati, lakini tunasisitiza halamashauri kutenga fedha za mapato ya ndani kuanza kukarabati stendi hii ya karatu, ahsante.