Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 37 2023-02-02

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya kisasa Ikungi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ina uhitaji wa stendi ya mabasi yenye ubora itakayowezesha huduma bora za usafiri.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri imekwishalipa fidia ya eneo la ukubwa wa hekari tano kiasi cha shilingi milioni 36 lililopo katika Kijiji cha Muungano Kata ya Unyahati ili kupisha ujenzi wa stendi hiyo.

Mheshimiwa Spika; katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023, Halmashauri imetenga kiasi cha shilingi milioni 110 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi hiyo.