Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa katika maeneo ambayo hayana mawasiliano katika Jimbo la Handeni Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN M. SALLU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Kata ya Sindeni pana Kituo cha Afya cha Tarafa ambako mawasiliano ni shida kabisa. Vilevile katika Mji wa Mkata ambako ni Makao Makuu ya Halmashauri, imejengwa Hospitali ya Halmashauri pamoja na Makao Makuu ya Halmashauri kilometa nne tu kutoka katikati ya mji, lakini mawasiliano yanasuasua: Je, ni lini Serikali itafanya hatua za makusudi kabisa kuhakikisha taasisi hizo za kiserikali zinapata mawasiliano ili mifumo ifanye kazi na wananchi kupata huduma stahiki haraka iwezekanavyo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ushirikiano wake mzuri ambao ametupatia hasa pale nilipofanya ziara katika Jimbo lake. Katika eneo hili ambalo ni la Sindeni, natambua kabisa kwamba kuna changamoto ya mawasiliano ambapo kulikuwa na mnara uliokuwa umejengwa kilometa 21 kutoka Makao Makuu ya Kata ambao haukuweza kufikisha huduma ya mawasiliano maeneo ambapo hiki Kituo cha Afya kilipojengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuahidi kwamba wataalamu wetu wataenda pale, watafanya tathmini, watakapojiridhisha ni namna gani tufanye, basi tutaingiza katika mpango wa utekelezaji. Kwa upande wa Kata ya Mkata ni kilometa nne. Kwa aina ya spectrum ambazo tunatumia nine hundred na eighteen hundred, ukiangalia hapa bado iko katika range. Kikubwa hapa, tutaenda kuliangalia tatizo ili tuweze kuongeza nguvu ya minara iliyopo katika Kata hii ya Mkata ili kuhakikisha kwamba Halmashauri na Hospitali zilizopo katika maeneo haya ambayo ni kilometa nne, zinapata huduma ya mawasiliano bila kuwa na changamoto yoyote, ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa katika maeneo ambayo hayana mawasiliano katika Jimbo la Handeni Vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naipongeza Serikali na ninamshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kufanya ziara katika Jimbo la Mbulu Mji. Swali langu ni dogo: Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutekeleza mpango wake wa bajeti wa miaka miwili wa Kata za Gunyoda, Silaloda na Marang kuweka minara kwa kuwa alijionea hali halisi?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu kumtaarifu Mheshimiwa Mbunge wa Mbulu Vijijini kuwa kata hizo ambazo amezitaja tayari ziko katika mchakato wa zabuni ambayo imefunguliwa jana. Kwa hiyo, tunaamini kwamba mchakato wa evaluation utakapokamilika, tutaelewa kwamba ni mtoa huduma gani ambaye amepatikana kwa ajili ya Mbulu Vijijini? Ahsante. (Makofi)