Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 31 2023-02-01

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: -

Je, ni lini minara ya simu itajengwa katika maeneo ambayo hayana mawasiliano katika Jimbo la Handeni Vijijini?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetekeleza miradi mbalimbali ya kufikisha huduma ya mawasilianao katika Jimbo la Handeni Vijijini katika Kata za Kwamatuku ambapo umejengwa mnara wa Tigo katika Kijiji cha Kwamatuku; Kwamkonje ambapo umejengwa mnara wa Tigo katika Kijiji cha Kwamkonje; na Misima ambapo imejengwa minara miwili ya TTCL katika Vijiji vya Kibaya na Msomera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilifanya tathmini ya upatikanaji wa huduma ya mawasiliano katika Jimbo la Handeni Vijijini katika Kata za Kang’ata, Kwamgwe, Kwamkonje, Kwaruguru, Kwasunga, Mazingara, Mgambo, Misima, Ndolwa na Sindeni pamoja na vijiji vyake vyote. Ilibainika uwepo wa changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano ambapo utatuzi wake unahitaji ujenzi wa minara ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia matokeo ya tathmini hiyo, Serikali imeziingiza kata hizi katika zabuni ya mradi wa Tanzania ya kidigitali iliyotangazwa na imefunguliwa tarehe 31 Januari, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.