Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma za kipolisi jirani na maeneo ya wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa shehia yangu ya Fuoni ina matatizo makubwa katika eneo hilo, matatizo ya wizi na vibaka pamoja na wabakaji, maana kuna vibaka na wabakaji masuala mawili hayo muyaone.

Je, Serikali haioni haja kujenga Kituo cha Polisi katika eneo hilo? (Makofi)

Je, ni lini Serikali itaanza huo ujenzi katika maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Dau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa kujenga Vituo vya Polisi kwa kweli unaanzia kwa wananchi na mamlaka zao za Serikali za Mitaa. Kwa maana ya uwepo wa matukio ya wizi, udokozi kwenye shehia aliyoibainisha, nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika vikao vya Kamati za Usalama watakapojadili na kuona umuhimu wa kujenga Kituo cha Polisi, basi sisi Polisi Makao Makuu kwa maana ya IGP atatenga fedha kwa ajili ya kusaidiana na nguvu za wananchi kujenga vituo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kama Kamati ya Usalama ya Wilaya na Mkoa wataona umuhimu tuko tayari kuungana nao. Ni lini? Wakati wowote tutakapopata maombi hayo tutatekeleza mpango wa ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma za kipolisi jirani na maeneo ya wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Ipo ahadi ya Serikali ya kujenga Kituo cha Polisi Itigi. Kwa muda mrefu, majengo wanayotumia polisi sasa ni ya reli na ambayo reli sasa wanajenga. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Polisi daraja B Itigi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kweli Itigi ulikuwa Mji Mdogo lakini sasa unakua kwa kasi na unahitaji Kituo cha Polisi na ndio maana tayari tumeshamtuma Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ili kufanya uhakiki wa uwepo wa kiwanja, ukubwa wake ili kuleta mahitaji na michoro iweze kuandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho. Kwa hiyo Mheshimiwa niko tayari kufuatilia jambo hilo ili kuona kwamba linatekelezwa ili Mji wa Itigi uweze kupata Kituo cha Polisi kama alivyoomba cha daraja B.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma za kipolisi jirani na maeneo ya wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Mmtaa wa Mlandege ulioko Mjini Unguja kulikuwa na Kituo cha Polisi toka wakati wa ukoloni na pana maduka mengi ya wananchi, lakini kituo hicho sasa hivi kimekufa. Naomba Wizara iangalie tena kukifufua kituo kile kwa sababu ni mtaa wa maduka na umezungukwa na wananchi na maduka.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ushauri nimeupokea na tutaangalia. Ahsante sana.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma za kipolisi jirani na maeneo ya wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. ORAN M. NJENZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwa kuwa wananchi wa Kata ya Igoma, Wilaya ya Mbeya wameanza kujenga kituo cha kimkakati kwa kuhudumia kata jirani za Wilaya Rungwe, Wilaya ya Mbeya na Wilaya ya Makete ikiwemo Kitulo pamoja na TFC. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kuwaunga wananchi waliojenga mpaka Mtamba wa Panya ili wamalizie hicho kituo cha kimkakati angalau milioni 100 tu? Kama Serikali inaweza kuwapelekea hicho kituo kitafika hatua nzuri. Nashukuru sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunawapongeza wananchi wa Mbeya Vijijini pamoja na Mheshimiwa Mbunge wao kwa ushirikiano walioufanya na kuanza ujenzi wa Kituo cha Polisi Kata ya Igoma kama ilivyoelezwa na Mheshimiwa Mbunge. Ombi langu kwa uongozi wa Wilaya ya Mbeya wawasilishe maombi kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi ili kituo hiki kiingizwe kwenye mpango wa ujenzi kama ambavyo tumefanya kwenye maeneo mengine. Nashukuru.