Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 28 2023-02-01

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma za kipolisi jirani na maeneo ya wananchi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwatum Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa madhumuni ya kupeleka huduma za polisi jirani na wananchi, Jeshi la Polisi linatekeleza utaratibu wa kuwapangia kazi Wakaguzi wa Polisi kwenye maeneo ya kata na shehia zote hapa nchini. Mpaka sasa Wakaguzi wa Polisi 2,552 wameshapelekwa kwenye kata hizo 2,552 na...Sorry, naomba kurejea eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi linatekeleza utaratibu wa kuwapangia kazi Wakaguzi wa Polisi kwenye maeneo ya kata na shehia zote hapa nchini. Mpaka sasa Wakaguzi 2,552 wameshapelekwa kwenye kata na 288 wameshapelekwa kwenye shehia kwa upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, majukumu ya Wakaguzi wa Polisi wanaopangwa kwenye kata na shehia ni kusimamia hali ya ulinzi na usalama kwenye maeneo yao na kushirikiana na wananchi kuanzisha na kusimamia vikundi vya ulinzi shirikishi, kushiriki vikao na mikutano ya vitongoji, vijiji, shehia na kata na ward ili kutatua changamoto za uhalifu na migogoro katika jamii, pia hushiriki kwenye mikutano ya kamati za maendeleo za kata ili kutoa ushauri kuhusiana na masuala ya ulinzi na usalama, nakushukuru.