Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kurekebisha sheria ili ubakaji na ulawiti kwa watoto uwe na kifungu tofauti cha sheria?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina swali moja la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitendo vya ubakaji na ulawiti kwa watoto vimekuwa vikiongezeka siku baada ya siku, na utaratibu wa kuendesha mashtaka ya kesi za ubakaji na ulawiti kwa watoto kulingana na Sheria ya Ushahidi (Evidence Act) inampa mtoto mzigo wa kuthibitisha kwamba amebakwa ama amelawitiwa.

Sasa Serikali haioni umuhimu wa kufanyia mapitio Sheria ya Ushahidi ili kuhakikisha mazingira ya kutoa ushahidi katika kesi za ubakaji za watoto pamoja na kesi za ulawiti kwa watoto zinawekewa mazingira zinazolinda haki za Watoto katika kesi hizo? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu swali la Mheshimiwa Judith Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama alivyouliza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba matendo ya ulawiti kwa watoto na ubakaji yamekuwa yakikithiri, lakini halitokani na mapungufu kwenye sheria.

Moja, sheria kwenye makosa ya jinai, uthibitisho au threshold ya kiwango cha uthibitishaji wa makosa ya jinai ni beyond reasonable doubt yaani uthibitishe pasipo kuacha shaka yoyote na nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kuliona hili na akaunda Tume Maalum ya Haki Jinai ambayo jana ilifanya kazi hiyo, ikiwa mojawapo ni kuhakikisha kwanza vyombo vyetu ambavyo ni functionalize of the law ambapo ni Ofisi ya Mwendesha Mashtaka, Polisi ambao ndio wanawajibu kwanza wa kupokea ripoti ya uhalifu wa utendekaji wa kosa, lakini pili kufanya uchunguzi; na tatu kupeleka sasa kupitia Ofisi ya Solicitor General kupeleka mashtaka mahakamani; na nne kazi ya mahakama kwa maana ya dispensational of justice.

Sasa changamoto ya mambo haya na ukizungumzia na Sheria ya Ushahidi alivyoieleza Mheshimiwa iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2004, sheria hii inaeleza kiwango cha uthibitishaji ni pasipokuacha shaka, kwa sababu ukiacha hivyo athari yake kuna watu wanaweza wakaumizwa kwa sababu ya kesi za kutengeneza. Ushahidi umeonekana unaharibika kwanza katika ngazi ya upelelezi, watoto wanafanyiwa matendo haya na wakati mwingine kunakuwa hakuna ushahidi kwa mfano ujazaji wa PF3, na kesi inavyoenda kule inakuwa imeharibika, lakini eneo lingine la uharibifu wa mashauri haya na kushindwa kuthibitisha ni pale ambapo waendesha mashtaka au wale wazazi kunapokuwa na dhamana, yule mtuhumiwa anatoka nje na anaharibu ushahidi. Wapo ambao ushahidi unaeleza wamekuwa waki bargain na wazazi na wanalipana huko na matokeo yake haendi mahakamani kwenda kutoa ushahidi na mahakamani huwezi ukashinda kesi bila kuwa na ushahidi.

Mheshimiwa mwenyekiti, pili; inatokea katika mazingira ambayo sheria zetu katika usimamizi wake ile enforcement katika dispensational of justice namna ya utoaji wa ushahidi kwa watoto wadogo, nimkumbushe tu Mheshimiwa Judith Kapinga kwamba Sheria ya Ushahidi inatoa usikilizaji wa mashauri haya in camera, kwamba hayasikilizwi kwenye public hearing kwa maana ya aibu na kutunza ile heshima ya mtoto. Kwa hiyo, wale wasaidizi wake wanaweza wakamsikiliza na bado Sheria hiyo ya Ushahidi inatoa haki pia ya kupima uwezo wa mtoto kama ana uwezo wa kutoa ushahidi mahakamani au mtu mwingine aweze kusimamia hilo.

Kwa hiyo, kwenye eneo la Sheria ya Ushahidi bado tutaweza kuona kama kuna mapendekezo ambayo anayaona, nishukuru tu kwamba ameweza kuliona tutayachukua na kuweza kushauriana na mamlaka kuweza kuona maeneo gani ambayo tunafikiri sheria ina mapungufu na kwa kufanya tu hilo hata Wizara ya Maendeleo ya Jamii tayari wamekwishakaa kikao na kuona kama tunaweza tukaondoa dhamana kwenye makosa ya aina hii, ahsante.