Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 26 2023-02-01

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kurekebisha sheria ili ubakaji na ulawiti kwa watoto uwe na kifungu tofauti cha sheria?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 inaainisha ubakaji na ulawiti kuwa ni makosa ya jinai. Kwa mujibu wa sheria hii, kosa la ubakaji limeainishwa chini ya kifungu cha 130 na adhabu yake imeainishwa kwenye kifungu cha 131. Aidha, kosa la ulawiti na adhabu yake zimeainishwa chini ya kifungu cha 154 cha sheria hii. Makosa yote mawili yametolewa adhabu tofauti kulingana na mazingira na namna kosa lilivyotendeka. Adhabu ya chini kwa makosa hayo ni kifungo cha miaka 30 na adhabu ya juu ni kifungo cha maisha jela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vifungu hivyo makosa yote mawili yanapotendeka kwa mtoto chini ya miaka 10 adhabu yake ni kifungo cha maisha jela, pia adhabu hizo zinaweza kuambatana na kulipa fidia kwa kiwango kinachoamuliwa na Mahakama, ahsante. (Makofi)