Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawalipa mafao waliokuwa Wafanyakazi wa Viwanda vya Kilitex na Sunguratex Gongo la Mboto?

Supplementary Question 1

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, kwa kuwa suala hili limekuwa likijitokeza mara kwa mara. Je, Naibu Waziri atakuwa tayari kuambatana na mimi kwenda kukutana na wafanyakazi hawa ambao wana malalamiko ya muda mrefu ili kuweza kuwapatia majibu waweze kufunga shauri hili mara moja?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kama nilivyoeleza na kujibu kwenye swali la msingi kwamba sisi tuko tayari kuweza kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mheshimiwa Mbunge ili kwenda kutatua changamoto za wafanyakazi hawa na kuweza kulifanyia uchunguzi wa kina, kama wapo wanaostahili kulipwa basi watalipwa na tutaweza kilifanyia kazi.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawalipa mafao waliokuwa Wafanyakazi wa Viwanda vya Kilitex na Sunguratex Gongo la Mboto?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kiwanda cha Nyuzi pia Tabora kina matatizo kama ambayo yapo kule Ukonga. Wafanyakazi waliachishwa muda mrefu lakini wengi hawakupata mafao yao. Nilikuomba Mheshimiwa Waziri kama utakuwa tayari tuambatane ukawa umeniahuidi lakini mpaka leo naona bado sijui lini utakuwa tayari ili ukawasikilize wale wafanyakazi, kwa kweli hali zao ni mbaya sana, ahsante.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka ambaye kimsingi ameeleza pia hali ya changamoto zilizo katika viwanda vilivyokuwa kama Kilitex pamoja na Sunguratex, hali hiyo ipo pia kwenye Kiwanda cha Nyuzi kule Tabora. Mimi nipo tayari kuweza kushirikiana naye hata kuambatana nae ili kuweza kutatua changamoto hiyo lakini katika hatua ya awali pia tutapata nyaraka na idadi ya majina hayo ili tuweze kuona urahisi zaidi wa kuwahudumia wananchi wetu, ahsante. (Makofi)