Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 20 2023-02-01

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawalipa mafao waliokuwa Wafanyakazi wa Viwanda vya Kilitex na Sunguratex Gongo la Mboto?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka 1989 Serikali kupitia Mifuko ya NSSF uliokuwa PPF iliwalipa mafao waliokuwa wafanyakazi wa viwanda vya Kilitex na Sunguratex Gongo la Mboto baada ya ukomo wa ajira zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Aprili, 2022 Mfuko wa PSSSF ulipokea malalamiko ya waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda Sunguratex wapatao 644 wakidai kuwa hawakulipwa mafao kikamilifu na uliokuwa Mfuko wa PPF. Baada ya Mfuko kufanya uchambuzi wa madai hayo, imeonekana kuwa wafanyakazi hao walishalipwa mafao kikamilifu isipokuwa baadhi yao wanasubiri kufikisha miaka 55 ili waanze kulipwa pensheni ya mwezi. Kuhusu wafanyakazi wa kiwanda cha Kilitex Mfuko haujapokea malalamiko yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipo tayari kuendelea kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine kama wafanyakazi hao wapo ili kutatua changamoto ya waliokuwa wafanyakazi wa viwanda vya Kilitex na Sunguratex Gongolamboto. Ahsante.