Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: - Je, ni makundi gani yamenufaika na mkopo wa shilingi trilioni moja iliyoahidiwa kutolewa na Serikali katika sekta ya kilimo na kwa masharti gani?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri wa Fedha mpaka sasa inaonekana ni shilingi bilioni 100 ndizo ambazo wananchi wameweza kukopeshwa na kuwafikia walengwa hao wa kilimo.

Je, Serikali haioni kwamba kama ulivyosema jibu la msingi, Serikali inakopesha taasisi na asasi za fedha kwa asilimia tatu lakini wakulima hawa wanakopeshwa kwa asilimia 10 ambazo ni kubwa sana na hatuwezi kuwasaidia wananchi wetu wa kawaida. Kwa nini Serikali isishushe na wananchi hawa wakapata kwenye asilimia Tano ili iweze kuwa na tija kwa wakulima wa Tanzania?

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, tunafahamu asilimia zaidi ya 70 ni wakulima hapa Tanzania, hatuoni kuna haja sasa ya kuhakikisha kutoka shilingi trilioni moja zimetoka tu, wewe unatamka hapo shilingi bilioni 160 ni ndogo, zaidi ya shilingi bilioni 800 bado hazijafika.

Je, hauoni sasa kuna haja, Serikali ihakikishe ahadi iliyosema kwenye shilingi trilioni moja angalau shilingi bilioni 900 tuweze kuwasaidia wakulima wa Tanzania?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii na nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake ya nyongeza lakini naomba niweke kumbukumbu sawa.

Mheshimiwa Spika, mikopo hii hawakopeshwi kwa asilimia 10, nilichosema wanatakiwa wakopeshwe kwa kiwango kisichozidi asilimia 10, kwa hiyo tulichokiweka ni asilimia Tisa kushuka chini. Tulichosema atakayepata fursa hiyo kutoka Benki Kuu anatakiwa awakopeshe wakulima kwa single digit, kwa riba ya asilimia isiyozidi kumi, kwa hiyo ni tisa kushuka chini na hicho ndicho ambacho kimekuwa kikifanyika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kiwango, tofauti na fedha zingine ambazo tuna-finance project, hii hapa inatoka kufuatana na uhitaji, kwa hiyo kadri benki zinavyochukua na kadri wahitaji wanavyochukua, ndivyo kiwango hiki kinavyoendelea kuwa kikubwa. Kwa hiyo, kwa kuwa Bunge ni sehemu ya viongozi tunaoongoza wananchi tuendelee kuweka hamasa. Hili linaendana sambamba kabisa na jinsi ambavyo hii sekta ya kilimo imekuwa na uamsho kuhusu masuala ya kutumia benki.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)