Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 18 2023-01-31

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: -

Je, ni makundi gani yamenufaika na mkopo wa shilingi trilioni moja iliyoahidiwa kutolewa na Serikali katika sekta ya kilimo na kwa masharti gani?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania ilichukua hatua za ziada za kisera, ikiwemo kuanzisha dirisha la mkopo maalum la shilingi trilioni moja kwa benki na taasisi za fedha nchini ili kuchochea mikopo nafuu kwa sekta binafsi, hususan sekta ya kilimo. Masharti ya mkopo maalum ni kuchochea mnyororo wa thamani katika kilimo cha mazao, miundombinu ya umwagiliaji, mifugo, uvuvi na ununuzi na usindikaji wa mazao kwa wakulima wadogo na wa kati pamoja na kampuni ndogo ndogo na za kati. Aidha, benki na taasisi za fedha zinatakiwa kutoa mkopo usiozidi shilingi bilioni moja kwa kila mkulima kwa riba ya asilimia chini ya asilimia 10.

Mheshimiwa Spika, masharti mengine ni Benki Kuu kuzikopesha benki na taasisi za fedha kwa riba ya asilimia Tatu ili taasisi hizo kukopesha wakulima na kampuni zinazojishughulisha na mnyororo wa thamani katika sekta ya kilimo kwa riba isiyozidi asilimia 10. Aidha, hadi tarehe 31 Desemba, 2022, jumla ya mkopo wa shillingi billioni 164.9 umetolewa kwa sekta ya benki na taasisi za fedha na kuwanufaisha wakulima wadogo na wakulima wa kati zaidi ya 5,385 na AMCOS 21.