Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali katika kuziendeleza timu za michezo za watoto?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, michezo sasa ni ajira na Wizara kwa maana ya Serikali ina mpango wa kujenga shule 56 nchini ambazo ni academies kwa ajili ya shughuli za michezo.

Je, ni lini sasa ujenzi wa shule hizi utaanza?

Mheshimiwa Spika, ningependa pia kujua katika shule 56 ambazo ni sports academies zitakazojengwa nchini, ni shule ngapi zitajengwa katika Mkoa wangu wa Tanga? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA SANAA, UTAMADUNI NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Husna Sekiboko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Husna kwanza amependa kufahamu ni lini ujenzi wa shule hizi 56 teule utaanza. Naomba niliarifu Bunge lako tukufu kwamba ujenzi wa shule hizi umeshaanza na tunashukuru Bunge lako tukufu mlitupitishia zaidi shilingi bilioni mbili na sasa zaidi ya shule saba zimeshapitiwa na ujenzi umeanza na unaendelea.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Husna alitaka kufahamu Mkoa wa Tanga katika hizi shule 56 teule za michezo una shule ngapi? Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba takribani Mikoa yote timu ambayo imetoka TAMISEMI, ambayo imetoka Wizarani kwetu na Wizara ya Elimu imeteua shule mbili kwa kila Mkoa, lakini kuna baadhi ya mikoa ina shule tatu kulingana na mazingira ya watu wenye uhitaji, lakini zaidi kila Mikoa ina shule mbili mbili.

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Tanga naomba nimtajie shule zake kwamba ni Tanga Technical Secondary School na Nyerere Memorial Secondary School pia katika mwaka huu miongoni mwa shule hizi saba, shule hii ya Tanga tunakwenda kuanza ujenzi maana tunategemea UMITASHUMTA na UMISETA tutahamia huko baada ya kutoka Tabora. Ahsante. (Makofi)