Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 17 2023-01-31

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, ni upi mkakati wa Serikali katika kuziendeleza timu za michezo za watoto?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kuthamini michezo ya watoto kwa kuwa umahiri wa timu mbalimbali unatokana na ushiriki mzuri wa watoto katika ngazi za chini ambazo hupelekea urahisi wa kuibua na kuendeleza vipaji. Serikali ina mkakati wa kuziendeleza timu za watoto kwa kuhakikisha kuwa kunakuwepo na mashindano mengi yanayohusisha watoto ili kuwajengea uzoefu.

Mheshimiwa Spika, sehemu ya mikakati hiyo ni pamoja na uendeshaji wa mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA, ukarabati wa miundombinu ya michezo katika shule 56 teule za michezo, pamoja na usajili wa vituo vya michezo ya watoto (sports academies). Aidha, Serikali imeendelea kuhamasisha wadau mbalimbali kuandaa mashindano ya timu za watoto na kuwajengea mazingira wezeshi ya kuendeleza vituo hivyo. Ahsante.