Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza migogoro ya Wafugaji na Wakulima katika Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, Serikali ina mikakati gani endelevu ambayo itakuwa imejiwekea ili kuepusha migogoro hii ambayo inapelekea wananchi wetu kuuana? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni hatua gani zinachukuliwa na Serikali kwa wale wanaobainika kusababisha migogoro hiyo? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imeendelea kufanya jitihada mbali mbali za kuhakikisha kwamba ina suluhisha migogoro hiyo ikiwemo kuendelea na programu za kupanga, kupima na kumilikisha lakini pia kuendelea kupanga bajeti kwa ajili ya kuhakikisha mipango yote inaendelea kupangwa katika maeneo hayo.

Pia, kushirikiana na mamlaka za upangaji, tumeendelea kuelimishana na kupanga bajeti kuhakikisha kwamba maeneo yote vijiji yanaendelea kupimwa na kupangwa ili kuondoa malalamiko ya wananchi ikiwemo migogoro hii inayoendelea katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa swali la pili lililoulizwa na Mheshimiwa Maimuna Pathan, juu ya hatua gani zinazofanyika kwa wale ambao wanaendelea kufanya fujo, jeshi letu la polisi limejidhibiti katika kuhakikisha kwamba watu wote wanaofanya matatizo au kuendeleza fujo katika maeneo yetu wanashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. (Makofi)