Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 15 2023-01-31

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza migogoro ya Wafugaji na Wakulima katika Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa Niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kumjibu swali lake Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Mkoa wa Lindi Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa migogoro ya ardhi katika Wilaya zote zilizotajwa ikiwemo Liwale, Nachingwea na Kilwa, lakini pia ni pamoja na maeneo ya Lindi Vijijini. Migogoro hii inatokana na kuongezeka kwa mifugo katika maeneo hayo, changamoto ya tafsiri ya mipaka ya ardhi katika vijiji hivyo, usimamizi mbovu wa mipango ya matumizi ya ardhi. Kwa kutambua hilo, Serikali imeendelea kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi ambayo kimsingi ndiyo suluhisho la migogoro ya mwingiliano baina ya watumiaji wa ardhi. Hadi sasa jumla ya vijiji 114 katika Wilaya ya Kilwa, Nachingwea na Liwale vimeandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2204, Serikali imepanga kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi katika vijiji 40 ikiwemo Liwale (17), Nachingwea (12) na Kilwa (11) katika Mkoani wa Lindi, ahsante.