Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya NIDA katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA OMAR KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi, kwanza naomba nikumbushe tu kwamba kwa Zanzibar tunatumia Wadi siyo Kata. Kwa hiyo, hii ni Wadi ya Kiuyu.

Mheshimiwa Spika, naomba niulize swali moja la nyongeza kama ifuatanyo; ni miaka miwili sasa tumekuwa tukipata matumaini haya ya Serikali kwamba tutajengewa ofisi, lakini kiukweli hali ni mbaya. Kwa NIDA Micheweni wanatumia vyumba viwili walivyoazimwa na Wizara ya Afya ambapo vyumba hivyo viwili wanatumia Ofisi ya DRO, Ofisi ya Picha, store na jiko. Kwa kweli hali mbaya sana, hata ufanisi unakuwa ni mdogo sana.

Mheshimiwa Spika, tunaomba commitment ya Serikali; je, ni quarter gani ya mwaka wa fedha husika tutaanza kujengewa ofisi hii wananchi wa Wilaya ya Micheweni? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kombo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kweli narekebisha, badala ya kuita Kata ya Kiuyu, ni Wadi ya Kiuyu, ahsante sana.

Kuhusu kuwapa matumaini na kwamba hali ya ofisi hizo ni mbaya sana, nakubaliana naye. Ndiyo maana tunasema katika mwaka 2023/2024 tutaweka fedha kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hii.

Mheshimiwa Spika, commitment ninayoitoa, ni kazi ndogo tu. Bunge lako tukufu likiidhinisha bajeti hii ambayo itakuwa imebeba pia dhima ya kujenga hizo ofisi 31, ni kwa uhakika kabisa jimbo lake litanufaika na ujenzi huo, ahsante.

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya NIDA katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Kaskazini B - Unguja ni miongoni mwa wilaya ambazo zimekosekana ofisi hiyo ya NIDA; je, ni lini Serikali itawahakikishia wananchi wa Wilaya ya Kaskazini B kuwajengea kituo hicho cha Ofisi ya NIDA? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juma Usonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natambua uwepo wa changamoto za ofisi maeneo mbali mbali ikiwemo wilaya aliyoitaja ya Kaskazini B, Unguja. Ni ahadi yetu tutaendelea kujenga hatua kwa hatua kulingana na upatikanaji wa fedha. Kama muda ungeruhusu, ningeweza kusoma hizo ofisi 31 ambazo zitapata fedha, lakini niko tayari kuzi-share na Waheshimiwa Wabunge wajue lakini kadri tunavyopata fedha, kila kusipokuwa na ofisi tutajenga ofisi hizo. Nashukuru.