Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 9 2023-01-31

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya NIDA katika Wilaya ya Micheweni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Jimbo la Wingwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kujenga ofisi 31 katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa gharama ya dola za Kimarekani 84,924,918 sawa na fedha za Tanzania shilingi 197,094,598,943.58. Fedha hizo zinajumuisha mchango wa Serikali wa jumla ya dola za Kimarekani 14,924,918 na mkopo nafuu wa dola za Kimarekani 70,000,000 kutoka Serikali ya Jamhuri ya Korea ya Kusini. Wilaya ya Micheweni iliyopo Mkoa wa Kaskazini Pemba ni mojawapo ya Wilaya zitakazonufaika kwa kujengewa Ofisi ya Usajili na Utambuzi wa Watu. Ofisi hiyo itajengwa kwenye Kiwanja Na. 10, kilichopo Shehia ya Maziwang’ombe, huko Micheweni, ahsante.