Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti matukio ya ubakaji wa akina mama uliokithiri katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ya kutoa elimu ninalo swali hili: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu matukio haya ya uvunjifu wa sheria kwa vitendo hivi ambavyo nimevieleza katika swali la msingi vimeanza kuwa na matukio mengi, na sasa hivi yanapelekea matishio hata kwenye shule zetu za msingi na sekondari: Je, kwa nini Serikali isianzishe kampeni ya kutoa elimu ambayo itakwenda kila maeneo kunusuru Taifa hii na vitendo hivi vya uvunjifu wa sheria?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Massay, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli anachokisema tumepata malalamiko kwamba baadhi ya matendo yanayokiuka maadili ya Taifa na jamii zetu yameingia hadi kwenye shule, siyo msingi, sekondari na pengine hata vyuo. Wizara ya Mambo ya Nchi kama Wizara yenye dhamana ya kusimamia sheria, ulinzi wa mali, watu na mali zao, na kukabiliana na makosa ya kijinai yakiwemo haya, inaendelea kuhimiza jamii nzima, kama tulivyosema mara kwa mara, makosa mengi ni matokeo ya vitendo vilivyoko kwenye jamii zetu. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa na ushirikiano kwa maana ya wazazi walezi jamii, shule, taasisi za dini na makundi mbalimbali kupigia kelele maeneo haya ili kuyatokomeza.

Mheshimiwa Spika, upande wa Jeshi la Polisi yeyote anayekiuka sheria ikiwemo kutenda makosa haya yanayobainika, uchunguzi unafanywa, tukithibitisha, wanapelekwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake. Kwa maana ya jamii nzima, nimeona juhudi zinafanywa na Wizara mbalimbali ikiwemo Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Wizara ya Elimu hili liwe jukumu letu sote kukemea matendo kama haya.

Mheshimiwa Spika, naungana na Mheshimiwa Mbunge kuhusu kutoa elimu kwa ujumla kwa nchi nzima ili kukomesha vitendo hivi ambavyo vinakiuka kwa kiwango kikubwa maadili ya nchi yetu, ahsante. (Makofi)