Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 8 2023-01-31

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti matukio ya ubakaji wa akina mama uliokithiri katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi linaendelea na jitihada zake za kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani watu wote wanaojihusisha na matukio ya uvunjifu wa sheria ikiwemo ya ubakaji. Aidha, Jeshi pia hutoa elimu kwa jamii kwa kuwashirikisha viongozi wa dini, mila na watu maarufu ili jamii iache kutenda makosa hayo. Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatoa wito kwa jamii yote kushirikiana kutokomeza matukio ya uhalifu hapa nchini yakiwemo ubakaji kwani yanasababisha athari kubwa kwa jamii, ahsante.