Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga josho katika Kata ya Miula Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza kabisa niipongeze Serikali kwa kutuletea pesa katika miradi hiyo aliyoitaja, Mradi wa Chala, Kate, Mtuchi, Kandasi na sehemu zingine zote. Hata hivyo miradi hiyo ni kama imetelekezwa. Wananchi wanalalamika hakuna kwa kupeleka ng’ombe kwenda kuogelea. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itaweka mkakati madhubuti wa kusimamia miradi hii iweze kutekelezeka?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Wilaya ya Sumbawanga DC ina mifugo mingi. Je, ni lini Serikali itajenga mabwawa ya kutosha kwa ajili ya mifugo? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ni mkakati gani wa Serikali juu ya kuhakikisha kwamba tunakuwa na umadhubuti kwenye usimamizi wa miradi hii? Tumejaribu kuona namna wa kurekebisha mfumo wetu na mfumo ambao tutakwenda nao katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 ni wa kupeleka fedha hizi moja kwa moja kwenye maeneo ya wanufaika, kwenye vijiji ili waweze kusimamia miradi hii ambayo itakwenda kuwanufaisha wananchi wao wenyewe moja kwa moja. Ambapo kwa sasa tunatumia mbinu ya kwamba miradi inalipwa na Wizara ingawa inasimamiwa na Halmashauri za Wilaya. Kwa hiyo tunaamini kwamba baada ya kuboresha mfumo huu sasa hakutakuwa na uzubaifu tena wa miradi yetu.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, ni lini tutapeleka miradi mipya ya mabwawa kwa kuwa kuna ng’ombe wengi kule Nkasi? Naomba Mheshimiwa Bupe atupatie haya maeneo ili tuangalie katika bajeti hii ya mwaka huu kama tunaweza pia kupeleka miradi hii katika Jimbo la kule Nkasi.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga josho katika Kata ya Miula Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Jimbo la Kalenga tulileta maombi matatu ya kujenga majosho katika Kata ya Kiwele, Mgela, Saadani pale Masaka pamoja na Ifunda Udumuka.

Je, ni lini Serikali sasa itatuletea fedha hizo ili tujenge hayo majosho? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, anayetaka kufahamu ni lini Serikali itakamilisha miradi ya majosho katika vijiji alivyovitaja kwenye Jimbo la Kalenga.

Mheshimiwa Spika, tumeshapeleka jumla ya fedha, shilingi bilioni 5.4 katika Halmashauri 80 na tumebakiza kiasi kidogo cha takribani shilingi milioni 500 ambapo tunataka twende kukamilisha hivi sasa. Mheshimiwa Kiswaga nitaomba baada ya Bunge unipatie hivyo vijiji ili nitazame kuona kwamba kama ni katika vile vilivyosalia na hatimaye viweze kupata fedha na miradi ile iweze kukamilika.

Name

Christopher Olonyokie Ole-Sendeka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga josho katika Kata ya Miula Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 3

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Wizara ya Mifugo ikiongozwa na Waziri na wewe Mheshimiwa Naibu Waziri, mlikuja wakati wa janga la mwaka 2020 la ukame Wilayani Simanjiro na kushuhudia vifo vya mifugo mingi, mliahidi kutokana na upungufu wa majosho tuliokuwa nayo mtatujengea au mtatoa fedha ya majosho 20; kinyume chake, bajeti iliyofuata mwaka 2021 mmetupa majosho mawili.

Je, lini sasa Serikali itatoa hizo shilingi milioni 400 ili kukamilisha majosho yale ambayo yataungana na nguvu za wananchi ili kuepusha vifo vya mifugo katika nyanda hizo kame?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ole-Sendeka Mbunge wa Simanjiro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika maeneo ambayo yamekuwa yakiathirika kwa kiasi kikubwa na ukame ni pamoja na Mkoa wa Manyara hasa Wilaya ya Simanjiro na Wilaya ya Kiteto. Katika bajeti ya mwaka huu, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa majosho na mabwawa.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Ole- sendeka atupatie vile vijiji ambavyo wamekubaliana viende vikajengewe majosho ili kusudi Serikali iweze kutekeleza kazi hii ya kuhudumia wafugaji, ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga josho katika Kata ya Miula Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 4

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; tatizo la majosho lipo pia katika Jimbo la Geita Mjini na majosho yaliyopo yanashindwa kufanya kazi kwa sababu hayana maji.

Je, Wizara ina mkakati gani wa pamoja kwamba pale ambapo kuna majosho panakuwa na maji ya uhakika ili majosho yaweze kufanya kazi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni mkakati gani wa Serikali wa kuhakikisha kuwa tunakuwa na maji ya uhakika katika yale maeneo? La kwanza, haya maeneo huteuliwa au huchaguliwa na wananchi wao wenyewe kwa maana ya kwamba tunakwenda kujenga josho kulingana na matakwa ya wananchi, kulingana na mazingira yao.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali imeendelea kujenga visima virefu na mabwawa katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo, kama lipo josho ambalo kwa hakika kabisa liko tatizo la maji kwenye eneo hilo, hususan katika Jimbo la Mheshimiwa Kanyasu alikotaja hapo Geita, tunaomba jina la kijiji hicho ili tutazame katika bajeti zetu ili wananchi wale waweze kupata huduma hiyo.

Mheshimiwa Spika, vile vile mkakati wetu wa Serikalini ni kuungamanisha huduma hizi za maji kati yetu Wizara ya Mifugo na wenzetu wa Wizara ya Maji ili kusudi pale penye maeneo ambayo huduma ya maji kwa ajili ya binadamu ipo, pia huduma hiyo iweze kwenda kuhudumia mifugo.