Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: - Mpango wa TASAF kwa Zanzibar umenufaisha kaya 216, Unguja Shehia 204 na Pemba Shehia 78 ambapo ni sawa na 70% ya Shehia zote Zanzibar. Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Shehia zote 388 Zanzibar zinanufaika na mpango wa TASAF kwa 100% badala ya 70%?

Supplementary Question 1

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nina masuala mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; nje ya utoaji wa rasilimali fedha kwa kaya maskini je, ni mambo gani mengine Mpango huu wa TASAF unafanya kuzinufaisha kaya maskini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, mpango huu unategemea kuisha lini ili kaya maskini zinazonufaika zipate kujiandaa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza, kwamba TASAF imefanya nini kingine cha ziada kwa walengwa? TASAF imefanya mambo mengi ikiwemo kuingia MOU na Bodi ya Mikopo Tanzania ili kuweza kutoa mkopo wa asilimia 100 kwa wale wote ambao wanakwenda kwenye elimu ya juu kutoka kwenye kaya hizi za walengwa wa TASAF. Vilevile TASAF imewawezesha walengwa hawa kuwa na bima ya afya. Bima ya afya hii inawawezesha wao kupata matibabu wakati wowote hata pale ambapo wanakuwa hawana pesa. Vile vile mradi huu umejenga miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye madarasa, vituo vya afya na zahanati.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, mpango huu kwanza nilijulishe Bunge lako tukufu ulikuwa unaisha mwaka huu 2023. Hata hivyo, kwa jitihada zake Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwa mapenzi yake kwa Watanzania ameweza kutafuta fedha na kuongezea mradi huu fedha na sasa utakwenda mpaka 2025.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: - Mpango wa TASAF kwa Zanzibar umenufaisha kaya 216, Unguja Shehia 204 na Pemba Shehia 78 ambapo ni sawa na 70% ya Shehia zote Zanzibar. Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Shehia zote 388 Zanzibar zinanufaika na mpango wa TASAF kwa 100% badala ya 70%?

Supplementary Question 2

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri yangu ya Kaliua kuna walengwa wa TASAF wapatao 946 ambao wametolewa kwenye mpango wa TASAF kwa kigezo kwamba wamehitimu ilhali hata uwezo wa kupata milo mitatu hawana. Je, TASAF wanaangalia vigezo gani ambavyo vinawapelekea hao walengwa wa TASAF kutolewa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rehema Migilla, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tathmini ilifanyika nchini kote ambapo kulikuwa kuna kaya 156,000 ambazo zilionekana zimeboreka kiuchumi. Hata hivyo, bado mwongozo ulikuwa haujatolewa kwa wadau na Halmashauri zote nchini ni namna gani bora ya kuweza kuwaondoa. Sasa nitakaa na Mheshimiwa Mbunge kuweza kuona hizi kaya 946 ambazo wametolewa ni walitolewa kwa vigezo gani, halafu nitampatia majibu yake.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: - Mpango wa TASAF kwa Zanzibar umenufaisha kaya 216, Unguja Shehia 204 na Pemba Shehia 78 ambapo ni sawa na 70% ya Shehia zote Zanzibar. Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Shehia zote 388 Zanzibar zinanufaika na mpango wa TASAF kwa 100% badala ya 70%?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Katika Jimbo langu la Sikonge, mwaka jana baada ya tathmini kufanyika kila kijiji kwa kushirikiana na Viongozi wa Vijiji, kuna orodha ambayo ilikubalika kwa pande zote mbili, lakini ilipofika Makao Makuu ya Wilaya wakapunguza idadi kwa nusu. Hao waliopunguzwa wana malalamiko makubwa sana dhidi ya uamuzi wa kuwaondoa kwenye orodha ya wafaidika wa TASAF. Je, Serikali kwa nini ilichukua hatua hiyo na itarekebisha lini hatua hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu uliokuwepo ni kwamba yale majina ambayo yote yanaondolewa imewekwa namna ya kukata rufaa kwa yeyote ambaye anaona anakidhi vigezo vya kuwepo kwenye Mpango huu wa TASAF. Hivyo, nashauri kwamba watu wa Sikonge ambao wanaona kwamba wanastahili kuwepo kwenye mpango huu waweze kukata rufaa na rufaa zile zinapelekwa TASAF Makao Makuu. Inatumwa timu ya wataalam kuweza kwenda kuhakikisha na kuona kama watu hao wanastahili na kuweza kurudishwa kwenye mpango. Vile vile kama kwa Mheshimiwa Migila nitakaa na Mheshimiwa Kakunda ili kuona jinsi ya wataalam wetu kuweza kwenda na kuiangalia hiyo tathmini kwa ujumla.