Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuongeza na kujenga maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika Hospitali nchini?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza Serikali kwa kutenga hiyo shilingi bilioni 2.04 kwa bajeti ijayo kujenga maeneo ya kusubiria wagonjwa, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza, changamoto ya watu kukosa sehemu za kusubiria wagonjwa inaikumba hospitali za Mkoa wa Dar es Salaam za Temeke, Amana na Mwananyamala. Maeneo ambayo yametengwa ni madogo sana kiasi kwamba idadi ya watu ni wengi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua maeneo ya watu kukaa wanaosubiria wagonjwa katika hospital hizo za Mkoa wa Dar es Salaam?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa changamoto ya watu kukosa sehemu za kusubiria wagonjwa inaikumba hospitali ya Taifa ya Muhimbili, hali ambayo imesababisha taharuki, wananchi wanaokuwa kule ndani ni wengi lakini hawana sehemu maalum za kukaa, kusubiria kupata huduma na kusubiria kuona wagonjwa.

Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi wake ili waondokane na kadhia hiyo ya kufukuzwa hovyo hovyo na Askari Mgambo kule ndani ya hospitali ya Taifa ya Muhimbili? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa hospitali ya Mwananyamala na hospitali ya Temeke wametenga kwenye bajeti ya mwaka huu kabla ya Juni watakuwa wamejenga maeneo hayo, lakini hospitali ya Muhimbili hiyo kadhia inatokana na kazi hiyo anayoisema Mheshimiwa Mbunge kwamba wamefunga pale OPD wanafanya renovation kujenga vizuri, lakini kujenga hiyo sehemu ya kungojea na kuna maeneo mengine ambayo yamefungwa kazi hiyo anayoisema Mbunge ikifanyika, kwa hiyo ndani ya miezi mitatu hiyo kadhia itakuwa imeondoka. Ahsante. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuongeza na kujenga maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika Hospitali nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mimi nishukuru kwamba Serikali imeona hii changamoto kwa sababu katika Mkoa wetu wa Iringa hili tatizo ni kubwa sana, hasa kwenye hospitali yetu ya Mkoa wa Iringa wananchi wanasubiria kwenye magereza, kwa sababu hakuna kabisa eneo lakini pia katika Wilaya ya Kilolo Mufindi hakuna maeneo ya kusubiria wagonjwa.

Mheshimiwa Spika, lakini mimi nilikuwa naomba labda niulize. Je, ni kwanini Serikali pengine iingie sasa ubia? Kwa sababu iko haja kuwepo hata na hosteli wale wanaosubiria wagonjwa wanalala nje kabisa kwa sababu ya matatizo ya sehemu za kusubiria wagonjwa wetu? Ahsante (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, nimemuelewa. Anachokizungumzia ni kwamba Hospitali yao ya Mkoa wa Iringa iko kwenye eneo dogo na upande mwingine wapo Magereza, ambao kumekuwa na mjadala mkubwa. Kwamba wataka hospitali ile ihamishwe ipelekwe sehemu nyingine kwenye eneo ambalo ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, lakini investment iliyofanyika kwenye eneo lile ni kubwa sana kiasi kwamba ukihamisha harakaharaka utadororesha huduma za tiba. Sasa nimuombe Mheshimiwa Mbunge wakati Mkuu wa Mkoa na Wizara tukijadiliana kabla maamuzi hayo hayajafanyika atupe Subira, kwa sababu kuna mambo ya muhimu kwanza yanafikiriwa kati ya TAMISEMI lakini pia na sisi Wizara ya Afya na masuala yote ya tiba ili tuweze kufanya huo uamuzi.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuongeza na kujenga maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika Hospitali nchini?

Supplementary Question 3

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, pale Muhimbili miaka ya nyuma katika bustani (gardens) zinazozunguka na zingine zilizo ndani kulikuwa na street lights lakini vilevile kulikuwa na sehemu za kupumzika kwa wagonjwa; badala ya kukaa kwenye wodi muda wote huwa wanatoka kupata fresh air huduma zile hazipo.

Je, ni lini Serikali inatarajia kuzirudisha huduma zile?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, bado naendelea kuwasisitiza Waheshimiwa Wabunge, hizo sehemu zipo na sasa zinafanyiwa renovation ambayo ndio inayoleta shida ambazo wabunge wa Dar es Salaam wanaziona. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge avumilie kwa muda mfupi sana, renovation inayoendelea itakamilika, na hata hayo ya nje yatakuwa yameongezeka zile sehemu za kupumzikia.