Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2023-01-31

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuongeza na kujenga maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika Hospitali nchini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na ujenzi wa Hospitali mpya kwenye Halmashauri ambazo hazikuwa na hospitali, ambapo mpaka sasa jumla ya hospitali mpya 127 zinaendelea na ujenzi. Aidha, kumekuwa na changamoto ya kukosekana kwa majengo ya Ndugu wa Wagonjwa kusubiria kuona wagonjwa katika hospitali hizo.

Mheshimiwa Spika, ili kutatua changamoto hiyo, Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024 itatenga bajeti ya shilingi bilioni 2.04 kwa ajili ya ujenzi wa sehemu za kusubiria wagonjwa kwenye hospitali 102 ambazo zinakamilisha ujenzi wa wodi za kulaza wagonjwa. Ahsante.