Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 1

MHE. ALEXANDER P. MNYETI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo langu siyo kubishana na Mheshimiwa Waziri kuhusu asilimia zinazopatikana pale Misasi. Kwa mtizamo wangu kwa sababu naishi huko, kutoka asilimia 40, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Waziri kwamba upatikanaji wa maji Misasi ni chini ya asilimia Nne hakuna maji, watu wanatafuta maji, hakuna maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Mkandarasi aliyetekeleza mradi huu naweza nikasema ni kandarasi ya kitapeli, na Wizara imerithi miradi mingi ya kitapeli ya sampuli hii kwenye Taifa letu. Wakandarasi wanachukua fedha, lakini hawatekelezi miradi iliyokusudiwa kulinga na mkataba. Mradi huu tangu mwaka 2013 leo ni miaka tisa, kupeleka maji kilomita 15 kutoka chanzo cha maji, imekuwa ni stori za hapa, stori za pale, stori za kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, ni lini upo tayari twende Misasi ukawaeleze hizi stori wananchi wa Misasi wewe mwenyewe kwa sababu Wabunge tumeshachoka, tumeshayaeleza mambo haya kila siku, mradi huu umesimama, Mkandarasi haeleweki, fedha ameshachukua, hakuna kinachoendelea site.

MWENYEKITI: Haya ahsante.

MHE. ALEXANDER P. MNYETI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, ni lini mtaanza kuyafuta makandarasi ya namna hii kwenye Taifa letu, kwa sababu tumejaribu kufuatilia, Mkandarasi huyu kote alikotekeleza miradi hii yote ni feki, hakuna anachokifanya anachukua fedha.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Alexander Mnyeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza lini kufuatana na mimi mara baada ya Bunge hili tutakwenda kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Wakandarasi feki, tayari Wizara imeshughulika nao ipasavyo, huyo unayemuongelea tutaendelea kumfuatilia pia tufanye kama tulivyofanya kwa wengine. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa maji kutoka mto Mavuje, kuelekea katika miji ya Kilwa Masoko na Kilwa Kivinje, ni lini utaanza kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mbunge wa Jimbo la Kilwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu ni mradi muhimu sana kwa Jimbo la Kilwa na tunafahamu namna ambavyo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia kwa karibu sana. Mheshimiwa Mbunge mradi huu tunakwenda kuutekeleza mwaka ujao wa fedha.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama hapa kwa ajili ya mradi mmoja tu, mradi wa Mwanga, Same, Korogwe. Ukitaja Moshi, katika Mkoa wa Kilimanjaro, Mji mkubwa unaofuata ni Same, lakini takribani ni miaka kadhaa toka tumepata uhuru same haijawahi kupata maji safi na salama na wanaogea maji ya kununua mpaka leo.

Je, ni lini sasa ule mradi ambao tuliambiwa ungekamilika mwaka jana Septemba utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally, Mbunge Viti Maalum kutoka Kilimanjaro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu wa Same -Mwanga ni mradi ambao ni mkubwa na umetumia fedha nyingi na sisi kama Wizara tumefuatilia kwa karibu na tayari kazi zinaendelea. Hivyo nipende kusema mradi huu utakamilika ndani ya wakati kwa namna ambavyo usanifu unaonesha.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, umenipandisha cheo nafaa kuwa profesa, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa Miji 28 ni mradi ambao ulikuwa unaifaidisha sana Geita Mjini na Geita Vijijini, lakini kila tukiuliza hapa tunaambiwa tunakamilisha makaratasi.

Je, Mheshimiwa Waziri, ni lini mradi wa Miji 28 ambao unalifaidisha Jimbo la Geita kwa Kata utaanza? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daktari Musukuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ya Miji 28 tayari tumefikia hatua nzuri sasa ya manunuzi na mradi huu unaelekea kwenye utekelezaji kabla ya mwezi Juni, 2022.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitoa takwimu za upatikanaji wa maji kwenye maeneo yote takribani nchini ambazo hazina uhalisia. Sasa ni lini Serikali itafanya rejea ili iweze kuja na uhalisia wa upatikanaji wa maji kwenye maeneo yetu nchini kuliko ilivyo sasa hivi? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la takwimu, ni suala la pana, pale tunaposoma takwimu 40 percent, maana yake kuna calculation zinazofanyika, zinazojumuisha mtandao wa mabomba, pamoja na namna ambavyo ukubwa wake umefikia katika eneo la usambazaji. Hivyo masuala ya takwimu, katika mifumo ya usambazaji wa maji yanahesabu zake, lakini kikubwa ninachoweza kusema tusiangalie tu hii takwimu, angalieni kazi inayofanywa na Wizara ya Maji, mabadiliko ni makubwa, mageuzi ni makubwa na tutaendelea kuwafikia wananchi wote kutoa huduma safi ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 6

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Nataka kufahamu Je, Serikali ni kwa kiwango gani inatakeleza mkakati wa hifadhi na matumizi endelevu ya maji, kama vile kujenga au kutengeneza miradi ya uvunaji maji ya mvua kama vile ilivyoainishwa kwenye ukurasa 36, 37(a)(3) cha Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zainab Katiba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miundombinu ya mabwawa ndani ya Wizara ya Maji, kwa sasa tuna mabwawa Sita ambayo yako kwenye utekelezaji, lakini tuna sanifu mbalimbali ambazo zinaendelea na nyingine zimekamilika na katika utekelezaji huo, tayari tunatarajia kuwa na bwawa kubwa la Kidunda, ambalo wenzetu wa DAWASA chini ya uongozi wa Cyprian tayari wamepata kibali cha kuweza kwenda kumpa kazi Mkandarasi pamoja na Mhandisi Mshauri na hawa wote wameshaenda kuoneshwa site na tunarajia lile Bwawa la Kidunda liweze kuwa ukombozi mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa hapa Dodoma Bwawala Farkwa na lenyewe pia tunaendelea kulifanyia kazi ili liwe ni jibu sahihi la miradi kuwa endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo yote ya nchi tunatarajia kuchimba mabwawa mengi. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ameweza kuruhusu zaidi ya shilingi bilioni 34 tunazitumia kwa ajili ya kuleta mitambo seti Nne kwa ajili ya kuchimba mabwawa, vilevile seti 25 za kuchimba visima na seti za kufanya utafiti wa maji chini ya ardhi ziko nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mitambo hii yote kuwasili nchini Waheshimiwa Wabunge, tutafikia Majimbo yote kwa urahisi na suala la kuvuna maji ya mvua litapewa kipaumbele na kuona kwamba linaenda kuleta uendelevu wa miradi.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Supplementary Question 7

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maji imekuwa ikijipambanua vizuri sana kwamba inafanya vizuri na sisi tumeona lakini wana mapungufu mengine ni makubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi navyosema Mikoa ya Rukwa, Mbeya, Songwe, miradi mingi inachelewa kwa sababu RUWASA hawana tender board. Bodi ya manunuzi haipo kabisa katika Mikoa hiyo na hii inasababisha miradi mingi inachelewa. Hivi navyosema Jimboni Songwe miradi mingi toka mwaka jana imesuasua kwa sababu tenda bodi ya pale Mkoani haipo na wanatumia tenda bodi ya kwa RAS pale.

Je, ni lini Serikali sasa itawezesha Mikoa kuwa na bodi ya manunuzi ili miradi iweze kuharakishwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Philipo Mulugo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, inapendeza wote tukiwa na ufahamu wa pamoja kwamba hizi bodi huwa zina ukomo wa muda wake, bodi nyingi zime-expire muda wake, tayari Mheshimiwa Waziri ameaanza kufanyia kazi na maeneo yote yatapata boards ambazo zitaharakisha utendaji wa kazi zetu.