Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 48 2022-04-12

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Mji wa Misasi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waaziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti Mbunge wa Misungwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Misasi ina vijiji Vinne (4) vya Inonelwa, Misasi, Mwasagela na Manawa na vinapata huduma ya maji kupitia visima virefu viwili pamoja na skimu za maji za mtandao wa bomba. Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Kata hiyo ni asilimia 40. Katika kuboresha huduma ya maji katika Kata ya Misasi, Serikali inaendelea na ujenzi wa mradi unaotoa maji kwenye bomba kuu la Mabale-Mbarika kwenda kwenye vijiji vya Kata hiyo ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 90 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamilika kwa mradi huo kutaboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Kata ya Misasi kufikia asilimia 80. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali itaendelea na upanuzi wa mradi huo ili kuhakikisha wananchi wote wa Kata ya hiyo wanapata huduma ya maji safi na salama na yenye kutosheleza.