Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri katika Wizara hii. Niombe na kuishauri Serikali ifanye hivyo kwa Mikoa yote ya Tanzania nzima ukizingatia wanawake wenzetu na wao wanatakiwa wazae katika uzazi salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la nyongeza liko hivi, Mkoa wa Mara, ni kati ya Mikoa yenye changamoto yenye uhitaji huu wa vyumba vya kujifungulia wanawake wenzetu wenye uhitaji maalum.

Je, Serikali ina mpango gani wa kwenda kujenga vyumba hivyo katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara ukizingatia ni Mkoa special alikotoka muasisi wa Taifa hili Baba yetu Mwalimu Julius Nyerere?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza maelekezo ya Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan hasa alipokuwa anatusisitiza kuhusu eneo la kupunguza vifo vya akina Mama na Watoto mojawapo ni eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala siyo kujenga maeneo maalum kwa ajili ya wao kujifungulia, lakini ni suala la ndani ya ramani yenyewe na huduma yenyewe ambayo akina mama wengine wote wanapata huduma ndani humo kuhakikisha kwamba kuna usaidizi mazingira infrastructure inawasaidia wao kuweza kupata huduma hiyo. Lakini kunakuwepo na vifaa ambavyo vinaweza vikawasaidia wenzetu wenye mahitaji maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Afya kwa kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI kwamba sasa Waganga Wakuu wa Mikoa yote wanapokwenda kufanya usimamizi shirikishi eneo hilo liwe sehemu yao ya hadidu rejea ya kufuatilia kuhakikisha kila Wilaya, kuhakikisha kila Kituo cha Afya kila Zahanati wamezingatia hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati zilizojengwa miaka ya 2000 vyumba vyake havikidhi hadhi ya kujifungulia kinamama kwa kuwa ni vidogo na vingine ni mfano wa corridor limewekwa pazia tu.

Je, Serikali haioni haja zahanati hizo za zamani kukajengwa wodi ya akina Mama ili kuendana na sera ya afya ya kinamama baada ya kujifungua wapumzike Saa 24? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ndiyo maana nimesema Serikali imeanza na imegundua tatizo hilo kwamba lipo na ndiyo maana kumekuwa na marekebisho yanayoendelea kwenye vituo mbalimbali. Nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika harakati za kupunguza vifo vya akina Mama na Watoto hayo anayoyasema yamezingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaona kuna fungu maalum kwa kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI, limekuwa likipelekwa kwa ajili ya kujenga hayo maeneo ya akina Mama kwa ajili ya kujifungulia.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa, changamoto kubwa kabisa inayokabili watu wenye ulemavu wanapokwenda hospitali hasa ni mawasiliano kati ya Daktari na mgonjwa, kwa sababu ulemavu unatofautiana.

Je, nini mkakati wa kuhakikisha kwamba Madaktari wanaelewa lugha za watu wenye ulemavu, kwa sababu wengine wanaongea kwa ishara? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme Mheshimiwa kwa kweli ameelezea suala siyo tu kusema ulemavu lakini ni wenzetu wenye mahitaji maalum kwa sababu kila mmoja ana mahitaji yake tofauti ukilinganisha na mwenzake. Na anasema mojawapo ya sehemu ni kwenye mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli kwa mfano kwenye hospitali ya Kanda ya Mkoa wa Mbeya tayari tumeanza process ya kuweka wale watu wanaoweza kutafsiri lugha kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum, tunaendelea sasa ku-roll out kuingia kila mahali. Lakini kwa kweli kuna shida kubwa hasa kupata watu wale wenye uwezo wa kufafanua lugha, kufafanua na mambo mengine hasa inapofika maeneo ya kitiba. Lakini Serikali inawekeza eneo hilo nguvu kuhakikisha hao watu wanapata huduma hiyo.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sera ya Taifa ya Afya inatamka kuwa kila Kijiji kinastahili kuwa zahanati, kila Kata inastahili kuwa na kituo cha afya, na kila Wilaya inastahili kuwa na hospitali ya Wilaya.

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha vijiji 22 vilivyopo katika Wilaya ya Longido Mkoa wa Arusha, ambavyo havina zanahanti wala kituo cha afya vinafikiwa na huduma hii?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema na inakumbukwa kwenye Bunge hili yalishatoka maelekezo kwa maana kwa Halmashauri zetu kwamba watenge bajeti wao wenyewe kwa maana ya kujenga zahanati kulingana na mapato yao, lakini bado Serikali inafikiria namna ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo yalishatoka kwamba utaenda utajenga kituo cha afya kwenye Kata lakini ukweli ukiangalia idadi ya watu eneo husika na mahitaji ya kituo cha afya kile kituo cha afya inakuwa kama kinatumika chini ya kiwango. Ndiyo maana tumekwenda kwenye kusema kila Tarafa ipate kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachukua mawazo ya Mheshimiwa Mbunge hasa ulipozungumzia Longido kwa sababu ukizungumzia Longido ni karibia mara 2.5 ya Mkoa wa Kilimanjaro. Kwa hiyo, kwa kuangalia Longido specifically tunaweza tukakaa kwa pamoja na tuone ni namna gani tunaweza kufanya kwa approach hiyo ili tuweze ku-treat kila eneo kulingana na changamoto za eneo husika bila ku-generalize. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa na changamoto kubwa ya kuwatambua watoto ambao wamezaliwa na ulemavu katika hatua za awali kutokana na uelewa usiokuwa wakutosha kwa wale ambao wanazalisha yaani Manesi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza elimu hiyo kwa kasi hasa vijijini ili mtoto atambuliwe katika hatua za awali kabisa na kuweza kusaidiwa kwa mfano kwenye mtindio wa ubongo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli anachokisema Mbunge, lakini nimuondoe wasiwasi, uelewa kwa manesi ni mkubwa, lakini kumekuwa kukitokea maeneo machache ambayo kweli watoto wanachelewa kutambuliwa hasa kwa mfano wa wenye autism na matatizo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri tutaendelea kuhakikisha elimu inakwenda na utaona sasa hivi kuna taasisi ambazo zinahamasaisha hayo maeneo ambayo kwa kweli yamekuwa na changamoto. Ukiona Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan ametenganisha Wizara ya Afya na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, ni kwa sababu vile kuna masuala mengine ni ya kijamii na sasa kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii tutahakikisha kwenye eneo la jamii sasa hata wale ambao wanaoweza jamii ikashirikiana na sisi kuwatambua kwa sababu bado tuna tatizo vilevile, kuna watu wanaozalia majumbani na wakati mwingine wasifike kwenye vituo vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kushirikiana wote kwa pamoja ninahakika tutaweza kutatua hayo matatizo na Mbunge uwe mmojawapo wa balozi wetu kuhakikisha eneo hilo linafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Supplementary Question 6

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali zetu nyingi katika Mkoa wa Arusha hususan zile zilizoko kwenye Wilaya za pembezoni zina uhaba mkubwa wa vifaa vya kujifungulia kinamama.

Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha vifaa hivi vinapatikana na vinatolewa bure kwa akina mama? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna maeneo yenye changamoto. Lakini Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kama ambavyo nimekwishaeleza hapa Bungeni hapo kabla ameshatoa Shilingi Bilioni 333.8 na kila mwezi imekuwa ikitoka Bilioni 15.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kumekuwa na shida kwenye eneo la manunuzi kuhakikisha kwamba zile fedha zinanunuliwa vitu na kuhakikisha zinafika eneo husika. Tutaenda kulitatua hilo na kuhakikisha tunatekeleza kama alivyosema. Kwa sababu sasa hivi tatizo siyo fedha, tatizo ni kasi ya kuhakikisha vifaa vinafika eneo husika. Ahsante sana.