Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 46 2022-04-12

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA K.n.y. MHE. STELLA A. IKUPA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kuna vyumba maalum kwa ajili ya kujifungulia wanawake wenye ulemavu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Alex Ikupa, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshalitambua tatizo hilo na kwa muda mrefu sasa marekebisho yamekuwa yakifanyika kwenye miundombinu isiyo rafiki kwa wanawake wenye ulemavu na tayari kwenye ramani mpya za ujenzi wa vituo vya afya, hospitali, ununuzi wa vifaa tiba, mahitaji kwa watu wenye mahitaji maalum yamezingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.