Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ukurasa 177, ipo barabara ya kutoka Same – Mkomazi - Umba Junction - Maramba hadi Tanga.

Je, ni lini upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utafanyika kwa barabara hii kuunganisha Mkoa wa Kilimanjaro na Tanga kupitia Wilaya ya Lushoto na Mkinga? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Je, ni lini Serikali sasa itakamilisha upembuzi wa kina na usanifu katika kipande cha kutoka Mlalo kwenda Umba Junction kuungana na barabara hii ambayo nimeishaitaja? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Same - Kisiwani kuja Mkomazi ilikuwa inajengwa kwa vipande. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Wabunge wa Mkoa wa Kilimanjaro hasa Mheshimiwa Mama Anna Kilango ambaye inamhusu sana barabara hii, kwamba barabara hii ambayo ina urefu usiopungua kilometa 92 inatangazwa yote kujengwa kwa kiwango cha lami na ipo kwenye hatua mbalimbali za kutangaza zabuni.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa swali lake la pili, kuhusu barabara hii ya Mlalo - Umba Junction Serikali inaanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 2

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Serikali hutumia fedha nyingi sana katika kutengeneza barabara, lakini barabara hizo kwa muda mfupi tu huwa zinamomonyona na kuota manyasi: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutenga fedha kwa ajili ya maintance ya barabara hizi ili kuzinusuru? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kamguna kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara nyingi ambazo ni za changarawe ama za vumbi ni kweli kwamba hazidumu kwa muda mrefu na ndiyo maana zinatengewa fedha kwa ajili ya matengenezo ya kila mwaka. Azma ya Serikali ni kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami, lakini barabara hizi ni gharama, kwa hiyo, inategemea na upatikanaji wa fedha. Kwa hiyo, zile barabara kubwa za mkakati ndiyo tutaanza kuzijenga kwa lami, lakini kadri bajeti itakavyoruhusu, mpango ni kuzijenga barabara zote kwa lami zikiwepo na barabara za Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 3

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa fursa hii. Mkoa wa Tanga haujaunganishwa na Mkoa wa Manyara pamoja na Mkoa wa Morogoro kwa barabara ya lami. Ni lini Serikali itajenga barabara Handeni – Kibilashi – Kiteto – Kondoa - Singida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niseme Serikali imepokea ushauri ulioutoa. Nikuhakikishie kwamba katika bajeti ijayo limezingatiwa na tutaendelea kuzingatia zaidi ili kuokoa hizi barabara ambazo tayari zimeshajengwa.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali la nyongeza la Mheshimiwa Reuben Kwagilwa Mbunge, nataka nikuhakikishie kwamba barabara hii ambayo tumeitaja kutoka Handeni - Kiberashi kwenda Kibaya ni barabara ya changarawe na tayari tupo kwenye hatua za manunuzi, kilometa 50 kuanzia Handeni kuja Kiberashi kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami; na kama taratibu zote zitakamilika, barabara hii itaanza kujengwa mwaka huu wa fedha. Ahsante. (Makofi)

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 4

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Nataka kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, barabara ambayo inaanzia Dumila kupita Turiani kupita Kata ya Negelo hadi Vibaoni Handeni, ni barabara muhimu sana. Kwa upande wa Morogoro imeshakamilika kwa kiwango cha lami: Je, ni lini kilometa 120 kwa kiwango cha lami itakamilishwa?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omari Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoiainisha imeshafanyiwa usanifu; na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kwa umuhimu wa barabara hiyo iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, hapo ni upatikanaji wa fedha tu, once tutakavyopata barabara hii itaanza kujengwa. Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Mkoa wa Tabora hadi leo haujaunganishwa na Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Songwe; na kipande muhimu kabisa ambacho kinaunganisha mikoa mitano ni kipande cha kutoka Ipole mpaka Rungwa ambacho usanifu wa kina ulikamilika na tayari shilingi bilioni tano zikatengwa mwaka huu.

Ni lini hiyo barabara itajengwa ili Mkoa wa Tabora na Mkoa wa Mbeya na Songwe ziunganishwe? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kipaumbele ni kuunganisha mikoa na mikoa na barabara aliyoitaja siyo tu kwamba ni mkoa, lakini pia ni kati ya zile barabara kuu kutoka Tabora - Ipole hadi Rungwa ambayo inaunganisha na barabara inayotoka Manyoni - Singida kwenda Makongorosi.

Mheshimiwa Spika, kipande cha Manyoni - Itigi kuja Rungwa tunategemea muda wowote kutangazwa; na kipande cha Ipole kuja Rungwa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami ili barabara hiyo ambayo inaunganisha siyo tu na Tabora, ila na mikoa mingi ya Kaskazini iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 6

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Bariri kwenda Hunyali na kwenda mpaka Mgeta ni barabara ambayo iko kwenye barabara inayotoka Mwanza kwenda Musoma na barabara inayokwenda Serengeti. Kipande hicho cha barabara Mheshimiwa Rais Samia alipokuwa Bunda tuliomba kwamba kipande hiki kijengwe kwa kiwango cha lami. Ni lini barabara hii itajengwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Bunda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hii ni ahadi ya Rais, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara inaendelea kuifanyia kazi ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kama Mheshimiwa alivyokuwa ameahidi. Kwa sababu hayo sisi kwetu ni maelekezo na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutatekeleza kama Mheshimiwa Rais alivyoahidi.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 7

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kuhusu ujenzi wa barabara ya kutoka Maramba kwenda Humba kwenda Mlalo. Ni ipi kauli ya Serikali juu ya kipande cha kuunganisha kutoka Maramba - Mashewa kwenda Old Korogwe mpaka Korogwe Mjini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoainisha ipo kwenye mpango wa kukamilisha usanifu wa kina wa barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge inayoanzia Old Korogwe hadi Mabokweni kama nimemwelewa. Nadhani ndiyo hiyo barabara; ipo kwenye ukamilishaji wa kufanya usanifu ili iweze kuanza kwa kiwango cha lami baada ya kukamilisha usanifu. Ahsante.

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Supplementary Question 8

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya kutoka Masasi - Nachingwea kwenda Liwale ni barabara ya mkakati: Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja inaanzia Mtwara - Mnivata - Newala hadi Masasi, ina urefu wa kilometa 210. Kilometa 50 atakubaliana nami zimeshajengwa; na tunavyoongea sasa hivi, tupo kwenye hatua za mwisho, African Development Bank wanaijenga hiyo barabara; na kuanzia mwezi Tisa ama wa Kumi hii barabara itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kilometa zote 160. Ahsante.