Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 68 2022-04-19

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuunganisha barabara za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Mwanaisha Ng’azi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mpango wa Serikali ni kuiunganisha mikoa yote kwa barabara za lami. Mkoa wa Tanga unapakana na Mikoa ya Pwani, Morogoro, Manyara, Kilimanjaro na nchi jirani ya Kenya. Tanga imeunganishwa na barabara zifuatazo: Tanga – Chalinze (Mkoa wa Pwani), Handeni – Tuliani hadi Magole (upande wa Mkoa wa Morogoro), Handeni - Kibilashi – Kibaya, (Mkoa wa Manyara), Tanga – Korogwe hadi Same (Mkoa wa Kilimanjaro) na kwa upande wa Kenya ni Tanga - Horohoro.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, zipo barabara nyingine ambazo zinaunganisha Mkoa wa Tanga na mikoa ya jirani. Ahsante.