Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa jibu la Serikali la mara zote ni kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya utengenezaji wa barabara hizo zilizotajwa lakini kwa kuwa pale ni eneo muhimu na kuna ajali nyingi zinatokea. Je, Serikali haioni kwamba tunaweza kutanua maeneo yale kama ambavyo imetanuliwa barabara ya pale Picha ya Ndege, Kongowe na Chalinze ili kuweza kupunguza msongamano wa eneo lile la Mlandizi?

Mheshimiwa spika, swali la pili, kama tatizo ni fedha na barabara hii inayozunguzwa, amezungumza barabara ndefu na mimi shida yangu ni pale Mlandizi, hatuwezi kuweka taa za haraka barabarani za kuongozea magari ili kupunguza misongamano iliyopo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Kibaha na sote ni mashahidi ambao wengi tunapita kwenye barabara hii. Kutokana na hoja ya Mheshimiwa Mbunge na jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia ni kweli tulichosema ndio mpango wetu wa Wizara, lakini Wizara baada ya kufuatilia tunajaribu kuangalia uwezekano, tutafanya study tuwe na mpango wa muda mfupi ili kupunguza ajali, lakini pia na msongamano.

Kwa hiyo tutaangalia kama njia sahihi na rahisi itakuwa ni kupanua barabara kwa maana ya njia nne kama sehemu nyingine ama kuweka taa ili kwanza kuokoa ajali, lakini pia kupunguza msongamano ambao sasa umekuwa ni adha kubwa kwenye hiyo barabara. Msongamano huo pia upo hasa katika hizi njia ndogo zinazotoka Bagamoyo kwenda Mzenga ambapo wananchi wengi sana wanachelewa kukatisha ile barabara na kuona magari makubwa tu ndio yanayopita kwa muda mrefu. Kwa hiyo, tumelichukua na Wizara tunachukua kwa umuhimu mkubwa ili kuokoa ajali na pia kupunguza msongamano. Ahsante.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kilomita 25 kwa kiwango cha lami katika maingilio ya Daraja la Sibiti kwa kuwa bajeti yake imetengwa mwaka huu wa bajeti? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunategemea kujenga barabara za maingilio zenye urefu wa kilometa alizozitaja kama 23. Barabara imeshakamilika na tuko mbioni kwa muda wowote tutakapokuwa tumekamilisha fedha kwa sababu tunaendelea na hiyo mipango ya kuhakikisha kwamba maingilio yale yanajengwa kwa kiwago cha lami. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango upo, tumeahidi na tutautekeleza kadri fedha zitakapopatikana, kama si mwaka huu basi mwaka wa fedha tutakaouanza.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa wananchi wa Makambako wana mategemeo makubwa sana katika eneo la Idofi ambako Serikali imekuwa ikiahidi kwa muda mrefu, je, ni lini watajenga one stop center na kumalizia fidia ambayo ilibaki kwa wananchi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Forodha cha Idofi ni kati ya vituo vingi vya Tanzania ambavyo tunategemea kuvijenga na tayari vilishaainishwa. Sasa hivi tunachofanya ni kupata fedha na kwanza kuwalipa fidia wale ambao wanapisha ujenzi na baada ya hapo tunaanza kujenga Kituo hiki cha Forodha pale idofi katika Jimbo la Makambako. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Napenda kuuliza, je, ni lini barabara ya mzunguko kwenye Manispaa ya Mororogoro kuanzia Juniour Seminary mpaka Kihonda itajengwa ili kupisha msongamano wa magari sehemu za Msamvu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum Morogoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kwa jinsia anavyofatilia ujenzi wa hii barabara ya mzunguko Morogoro. Taratibu bado zinaendelea za kufanya usanifu wa hiyo barabara ili kupunguza msongamano katika barabara kuu inayopita Msamvu kwenda Dar es Salaam. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mara usanifu utakapokamilika barabara hii itaanza kujengwa. Ahsante.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Je, ni lini Serikali itajenga kilometa saba kwa kiwango cha lami za barabara kati ya Nasio-Mutunguru- Masonga ili kuondoa shida zilizopo kwenye barabara ile? Nashukuru sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hiyo aliyoainisha Nansio Mutunguru yenye urefu wa kilomita saba ipo kwenye mpango mkubwa wa kujenga barabara ya lami. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango bado upo, utaanza tu pale ambapo fedha tutakuwa tumeipata na ujenzi huu tutaanza na kukamilisha hizo kilomita saba za lami katika Kisiwa cha Ukerewe.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini barabara ya Utegi hadi Kilongwe inayounganisha Nchi za Tanzania na Kenya kwa upande wa Rorya itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuna kila sababu ya kuunganisha barabara zetu za lami na nchi jirani, lakini tuna barabara za kawaida na barabara kuu. Barabara ambayo tumeunganisha na Kenya ni ile barabara kuu ambayo inatoka Tarime kwenda mpaka wa Kenya ambao tayari ni barabara ya lami. Hata hivyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa barabara hii inatumika sana na wananchi wa Rorya na Watanzania kupitia Utegi kwenda Rorya, barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami kadri Serikali itakapokuwa imefanya usanifu na kupata fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.