Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 66 2022-04-19

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mzunguko katika makutano ya Barabara ya Dar es Salaam, Morogoro na Bagamoyo kuelekea Mlandizi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Michael Constantino Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Makofia, Mlandisi hadi Mzenga kilomita 35, makutano ya barabara ya Dar es Salaam -Morogoro na Makofia- Mlandizi-Mzenga eneo la Mlandizi limesanifiwa kwa ajili ya kujenga barabara ya mzunguko yaani round about. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuanza ujenzi wa barabara ya Makofia – Mlandizi hadi Mzenga utakaohusisha na ujenzi wa round about katika eneo la Mlandizi. Ahsante.