Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili mafupi ya kuongeza: -

Mheshimiwa Spika, kupanda miti na kutunza miti ni mambo mawili tofauti. Hata hivyo, na mimi nilishiriki kupanda hiyo miti Wami-Ruvu. Je, kuna mpango gani ambao umewekwa madhubuti wa kutunza hiyo miti 96,500 iweze kustawi angalau asilimia 70?

Swali la pili; Chuo cha Kilimo SUA mnakishirikishaje katika utunzaji wa vyanzo vya maji na pia katika utunzaji wa uoto wa asili, hasa kwenye milima ya Uluguru ambako ndio kuna vyanzo vya maji ambavyo vimeharibiwa kwa wingi?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Charistine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma ambaye pia ni Mwenyekiti wetu wa Kamati ambayo inafanya vizuri sana. Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kama alivyosema naye alishiriki kupanda miti, hii miti sote tumepeana majukumu kuona kwamba haifi na itapona zaidi ya asilimia hizo 70 ambazo amezitolea mfano.

Mheshimiwa Spika, suala la ushirikishaji wa Chuo cha SUA Wizara tumekuwa tukishirikiana na wataalam mbalimbali katika makongamano na namna ya kuona tunabadilishana uzoefu. Hata hapa juzi tulikuwa na kongamano zuri pale Dar- es-Salaam, yote ni kuona kwamba, tunashirikisha wataalam mbalimbali ili tuweze kuona tunapata elimu nzuri kwa watendaji, vilevile kutoa elimu kwa wananchi kuona vyanzo vya maji inakuwa ni jukumu la wote, tunavitunza na vyanzo hivi vinabaki kuwa ni endelevu kwa sababu tuna miradi mikubwa ambayo inaendelea kutekelezwa kwa kupitia fedha za Wizara. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na wimbi la uharibifu wa vyanzo vya mito ya maji katika Wilaya ya Namtumbo kutokana na mifugo. Vyanzo hivyo vya maji ndivyo vinatiririsha maji katika Mto wa Luwebu, mto mkuu ambao unakusanyika na kukutana na Mto Kilombero ambao una-form Mto Rufiji na maji yake yanaenda kwenye mradi wa umeme.

Je, Serikali inaweza kusaidia kwenda kudhibiti uharibifu wa mifugo katika vyanzo hivyo vya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo haya yote anayoyataja tayari Bonde la Mto Ziwa Nyasa linafanyiwa kazi na tayari mipaka inaendelea kuwekwa ili kuzuia shughuli za kibinadamu kwa wafugaji na wale wanaofanya ukulima mdogomdogo.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mji wa Sikonge unategemea sana Bwawa la Maji la Utyatya ambalo lilijengwa mwaka 1959, kuna uchafuzi mwingi kwa kipindi kirefu, uchafu mwingi umeingia kwenye hilo bwawa. Mwaka 2017/2018 Serikali ilipanga shilingi milioni 400 kwa ajili ya kulisafisha hilo bwawa, lakini haikuleta fedha kwa sababu kuna maeneo ambayo yalitakiwa Halmashauri iweze kuyalinda vizuri na mpaka sasa hivi yameshalindwa vizuri.

Je, hizo fedha zitakuja lini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, chanzo hicho tutaendelea kuja kukifanyia kazi na Bonde husika tayari limeshapewa maagizo. Nami kwa kupitia Bunge lako tukufu naomba niendelee kusisitiza Wakurugenzi wote wa Mabonde waweze kuwajibika kwa sababu vyanzo hivi ni mkakati wetu kama Wizara kuona kwamba, tunavilinda ili viweze kutuletea uendelevu wa miradi ambayo tunaendelea kuijenga. (Makofi)

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante: -

Mheshimiwa Spika, kuna korongo la Mto Barai katika Kijiji cha Durgeda ambalo linaleta uharibufu katika chemchemi ya Mto Durgeda. Waziri alitoka mwezi huu wa Tatu katika neo lile alisema kwamba, utekelezaji ungeanza ndani ya mwezi mmoja.

Je, lini utekelezaji wa Mto huu Barai utaanza ili kuokoa chemchemi ya Mto Durgeda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel AwaCk, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, korongo hili ni moja ya maeneo ambayo Bonde la Mto Pangani wanashughulika nalo. Hivyo, niseme tu kwamba, shughuli zitaendelea na sasa hivi wapo kwenye maandalizi wanakuja kutekeleza majukumu yao.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, mbali ya watu kuharibu mazingira, I mean miti na kadhalika kwenye vyanzo vya maji, kumekuwa na wimbi kubwa la watu kwenda kujenga kwenye vyanzo vya maji kwenye mito na maeneo mengine hatimaye kusababisha maji kushindwa kupita kwenye mikondo yake na wengine ni vigogo tu.

Je, Wizara yako kushirikiana na NEMC mna mkakati gani madhubuti wa kuhakikisha watu hawaendi kujenga kwenye vyanzo vya maji?(Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nampongeza Mheshimiwa Ester kwa kuweza kufuatilia vyanzo vyetu vya maji. Maeneo haya namna yanavyojengwa tunayafanyia kazi siyo tu na NEMC, tuna Wizara ya Kisekta sasa hivi tunapita huko. Moja ya shughuli tunayofanya ni kukataza na kuondoa wale wote ambao wamejenga kandokando ya vyanzo vya maji. (Makofi)