Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 57 2022-04-13

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji katika Manispaa ya Morogoro?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jukumu mojawapo la kusimamia rasilimali za maji ni kudhibiti uharibifu kuhakikisha vyanzo vya maji vinahifadhiwa kwa ajili ya uendelezaji na uharibifu unadhibitiwa wakati wote. Katika Manispaa ya Morogoro, Serikali inaendelea na utambuzi wa maeneo ya vyanzo vya maji, kuweka mipaka na kuyatangaza kuwa maeneo tengefu. Hadi Desemba 2021, vyanzo vya maji kumi vimewekwa mipaka, hii ni pamoja Bwawa la Mindu ambacho kimetangazwa kuwa eneo tengefu.

Mheshimiwa Spika, vilevile, jumuiya za watumia maji Saba zinashiriki katika uhifadhi wa vyanzo vya maji katika maeneo yao. Pia, vilabu 10 vya michezo vya watoto vimeundwa katika Shule za Msingi ili elimu ya utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji na mazingira inatolewa kwa jamii. Aidha, hadi Machi 2022 jumla ya miche ya miti 96,500 imepandwa katika maeneo mbalimbali ya vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Spika, mkakati wa muda mrefu wa kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji ni kuimarisha Bodi za Maji za Mabonde ili ziweze kutekeleza Mipango ya Uhifadhi wa Vidakio vya Maji nchini kwa Mabonde yote likiwemo Bonde la Wami-Ruvu. Mipango hiyo imeainisha maeneo ya vipaumbele kwa ajili ya shughuli za uhifadhi wa vyanzo vya maji ikiwemo kupanda miti rafiki kwa maji kwenye maeneo ya vyanzo vya maji, kilimo cha makinga maji, urejeshaji wa uoto wa asili kwenye kingo za mito na udhibiti wa utiririshaji wa majitaka kwenye mazingira.