Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itafanikisha kampasi ya Tunduru kuanza rasmi masomo ya muda mrefu badala ya ilivyo sasa kwa masomo ya vitendo ambayo ni ya muda mfupi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kungu Mbunge wa Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi kwamba kampasi ile tayari ilishaanza kazi toka mwaka 2018/2019, lakini kozi ambazo zinatolewa pale ni zile za muda mfupi wanafunzi wetu wanapokwenda kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 tumetenga zaidi ya Shilingi Milioni 250 kwa ajili ya kuongeza miundombinu kwenye eneo lile. Katika mwaka ujao wa fedha tutatenga tena fedha zaidi ya Shilingi Milioni 300 kwa ajili ya kuongeza miundombinu ambayo itasaidia sasa chuo kile kiweze ku-operate katika masaa 24 kwa muda wote.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya michakato hii kukamilika tunatarajia baada ya miaka hii Miwili hadi Mitatu tutaweza kuanza kozi pale za muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Supplementary Question 2

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kisangwa kilichopo Bunda ndicho chuo pekee kinachotoa fani mbalimbali za ufundi na tatizo kubwa pale ni mabweni.

Je, ni lini Serikali itatusaidia kupata mabweni hayo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maboto Mbunge wa Bunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna changamoto kwenye Vyuo vyetu vya FDC lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 tumefanya ukarabati pamoja na upanuzi wa vyuo hivi vya FDC 54 kote nchini.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie katika kipindi kijacho tunaendelea na upanuzi huo ambapo tunaamini kabisa, chuo hiki cha Bunda kitazingatiwa katika ukarabati na upanuzi pamoja na haya mabweni tutaweza kuyafikia. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Supplementary Question 3

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Katika Kijiji cha Maneme Wilayani Nanyumbu kuna majengo ambayo yaliachwa na Kampuni ya ujenzi wa barabara na Serikali ya Kijiji iliyakabidhi majengo yale Wizarani.

Je, ni lini Wizara itatekeleza ahadi yake ya kufungua Chuo cha Ufundi katika Wilaya yangu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mhata Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli eneo hili la Mtambaswala ambapo Kampuni yetu ya ujenzi wa barabara ilikuwa na kambi, tayari imekabidhiwa kwa Wizara ya Elimu kupitia Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA). Mwaka jana mwezi Novemba, 2021 timu yetu ya wataalam ilikwenda kufanya tathmini ya eneo lile namna gani tunaweza tukaboresha, kwa maana kwamba ya kufanya ukarabati pamoja na kuongeza baadhi ya miundombinu ili kiweze kufunguliwa.

Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tayari tathmini tumeshafanya na tunatarajia katika mwaka ujao wa fedha, eneo lile tutakwenda kulifanyia kazi kuhakikisha kwamba Chuo kile kinafunguliwa. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Supplementary Question 4

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa, sasa ni miaka miwili toka Serikali itoe fedha za ukarabati wa Chuo cha Maendeleo Tango - FDC Mbulu na kwa kuwa tayari mradi wa awali umeshatekelezwa.

Je, ni lini Serikali yetu itatoa tena fedha ya ukamilishaji wa majengo hayo ya Chuo cha Tango FDC kwa awamu ya pili? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mbunge wa Mbulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika majibu yaliyopita katika Chuo cha VETA kule Bunda ni hivyo hivyo kwa upande wa wenzetu wa Tango.

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwanza katika fedha ambazo tulizipata za UVIKO – 19 zaidi ya Shilingi Bilioni 6.8 zimekwenda kununua vifaa kwa ajili ya vyuo hivi vya FDC (54) kote nchini, ambapo Chuo hiki cha Tango nacho vilevile kimezingatiwa.

Mheshimiwa Spika, vifaa hivi tayari tunavipeleka kwenye maeneo haya ya vyuo, vilevile upanuzi wa vyuo hivi tumeuingiza kwenye bajeti yetu ya mwaka ujao wa fedha. Kwa hiyo, maeneo haya yote tutakwenda kuyafanyia kazi kuhakikisha kwamba vyuo hivi vinatoa taaluma ile ambayo inatakiwa katika maeneo husika.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Supplementary Question 5

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru: -

Mheshimiwa Spika, je, ni lini sasa chuo cha ufundi VETA kwa Wilaya ya Kilolo kitajengwa kama ambavyo zimekuwa ahadi za Serikali kwa muda mrefu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni sera ya Wizara ya Elimu kwamba, katika kila wilaya tunakwenda kujenga chuo cha VETA. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa vile sasa tumekamilisha ujenzi wa vyuo vya VETA katika Wilaya 29 na vile vinne vya Mikoa ambavyo tunakadiria kunako mwezi Mei tutakwenda kumaliza katika mwaka ujao wa fedha tutaendelea na ujenzi katika maeneo ambayo bado vyuo havijaweza kujengwa. Ninakushukuru sana.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Supplementary Question 6

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru: -

Mheshimiwa Spika, ningependa kujua ni lini Serikali itafungua au chuo kikuu au tawi la chuo kikuu Mkoani Kagera kwa kuwa limekuwa ni hitaji la muda mrefu na ukizingatia tuna ardhi ya kutosha? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tuna mradi wetu wa heat ambao tunataraji tutaanza kuutekeleza katika mwaka ujao wa fedha, miongoni mwa maeneo ambayo ni focused zone ni katika Mkoa wa Kagera. Kwa hiyo, nikuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge katika maeneo ambayo tunaenda kujenga campus nadhani ilikuweko campus pale ambayo baadae ilikuja kufungwa, tunaenda kuifufua ili kuhakikisha kwamba Mkoa wa Kagera unakwenda kupata chuo hiki.

Vilevile tunafungua chuo kikubwa sana cha VETA katika Mkoa wa Kagera ambapo tunaamini chuo kile kitakuwa na hadhi vilevile ya chuo kikubwa hapa nchini. (Makofi)