Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 6 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 55 2022-04-13

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafungua tawi la Chuo Kikuu cha Sokoine Wilayani Tunduru kwani majengo yamekamilika kwa asilimia 65?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, kilikabidhiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru majengo na ardhi kwenye eneo lililokuwa Kambi ya Mkandarasi wa ujenzi wa barabara katika Kijiji cha Darajambili tarehe 17 Agosti, 2018.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine kilianza kutumia majengo ya kampasi ya Tunduru kama kituo cha mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sayansi ya Usimamizi wa Wanyamapori na Wanafunzi wa Shahada ya Kwanza ya Sayansi ya Misitu mwaka, 2018/2019.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na mpango wa kufanya ukarabati wa miundombinu na kuanzisha shughuli mbalimbali za kitaaluma, utafiti na ushauri wa kitaalam kwa lengo la kuiwezesha kampasi hiyo kufikia malengo ya kuanzishwa kwake.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.(Makofi)