Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga nyumba za Walimu katika Halmashauri ya Ikungi?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake kama anavyosema mwenyewe Milioni 100 kwa upungufu ambao upo ambao ni zaidi ya asilimia 62 itatuchukua muda mrefu sana kukamilisha ujenzi wa nyumba hizi, kwa sababu walimu wetu wanafanya kazi nzuri na tuliwajengea madarasa mazuri huko vijijini mbapo tunatakiwa wakae karibu.

Je, ni mkakati upi wa haraka wa kutafuta fedha za kutosha kuweza kumaliza tatizo hili ambalo limekuwa kubwa na linapunguza ari ya walimu kufanya kazi? (Makofi)

Swali la pili ni pamoja na kwamba juhudi zinaendelea za kupata Walimu lakini walimu nao ni wachache sana ambao hawa-fit idadi ya wanafunzi ambao tunao, kwa sababu Serikali imetangaza ajira za Walimu na kwa sababu Halmashauri ya Ikungi ina upungufu mkubwa.

Ni nini Serikali itafanya kuhakikisha kwamba inapunguza kabisa tatizo la idadi ya walimu ambao wapo katika Halmashauri yetu ya Ikungi? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatambua kwamba kuna changamoto na fedha ambazo zimetolewa katika Halmashauri ya Ikungi ni ndogo. Mkakati wa Serikali kwa mfano, kama sasa hivi moja ya mikakati ya Serikali ni kuhakiksha kila sekondari mpya tunayoijenga ama shule mpya tunajenga na nyumba za walimu na ninyi mmekuwa mfano three in one. Yote hii ni katika kukabiliana na changamoto ya nyumba za walimu.

Mheshimiwa Spika, tuna mikakati mingi ikiwemo kutafuta fedha na jukumu letu kubwa la sasa ni kuhakikisha tunamaliza kwanza ujenzi wa madarasa na shule latika maeneo yote yenye uhitaji, mara baada ya kumaliza hiyo hatua yetu ya pili ni kuhakikisha tunajenga nyumba kwa Walimu hususan katika yale mazingira magumu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu upungufu wa Walimu katika Halmashauri ya Ikungi nimhakikishie tu Mhehsimiwa Mbunge katika hatua ambazo tumeshatangaza ajira, Ofisi ya Rais, TAMISEMI sasa hivi tutaajiri Walimu 9,800 na katika hizo ajira 9,800 tutakazoajiri sehemu ya Walimu tutapeleka katika Halmashauri yako. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikuondoe shaka na hilo.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga nyumba za Walimu katika Halmashauri ya Ikungi?

Supplementary Question 2

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa nyumba za Walimu kidogo kidogo na kwa kuwa, zipo nyumba za Walimu ambazo zimejengwa kabla ya uhuru na mara tu hata baada ya uhuru na sasa hivi ni chakavu sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati angalau zile zilizopo ili kuboresha makazi ya Walimu? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Zodo Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya maelekezo ambayo ofisi ya Rais, TAMISEMI tumeyatoa katika Halmashauri zote nchini ni kuhakikisha wanatenga fedha za ndani katika mapato yao ya ndani ili kufanya ukarabati wa nyumba zote ambazo zipo za Walimu katika Halmashauri husika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hata hichi anachokizungumza Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ninaendelea kuagiza Halmashauri kutekeleza yale maelekezo ambayo Ofisi ya Rais TAMISEMI iliyatoa ya kutenga fedha ili kukarabati hizo nyumba za Walimu katika maeneo yote ambayo zimechakaa.

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga nyumba za Walimu katika Halmashauri ya Ikungi?

Supplementary Question 3

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, changamoto ya nyumba za walimu ambayo iko kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ni sawa na changamoto iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Igunga ambapo angalau tumeanza hatua ya kwanza tumejenga maboma.

Je, ni nini mkakati wa Serikali kukamilisha maboma haya ambayo ni nyumba za walimu kwa ajili ya kuwapatia malazi? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ngassa Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya mkakati wa Serikali ni kuendelea kutoa fedha na tumekuwa tukifanya katika maeneo ambayo wananchi wamekuwa wakijenga maboma, ikiwemo nyumba za walimu vituo vya afya pamoja na madarasa, kwa hiyo tumekuwa tukifanya hivyo. Hata hili analolisema ni kwamba Serikali tutaendelea kutekeleza na ndiyo maana moja ya kazi yetu kubwa sasa hivi ni kutafuta fedha kuhakikisha maboma mengi tunayafikia kwa kadri itakavyowezekana.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga nyumba za Walimu katika Halmashauri ya Ikungi?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, kuna upungufu mkubwa wa nyumba za Walimu katika Mkoa wa Simiyu kwenye shule za sekondari.

Je, ni lini Serikali itajenga nyumba hizo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi ni kwamba, moja ya mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunatafuta fedha ili tuendelee kujenga nyumba, hususan katika yale mazingira magumu huo ndiyo mkakati wetu.

Mheshimiwa Spika, hata katika bajeti ambayo tutakwenda kuipitisha kuna fedha tumetenga kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika maeneo yale ambayo ni magumu. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kupeleka fedha kwa kadri ya mahitaji na tutagawanya kwa nchi nzima ili kuhakikisha tunaleta usawa kwenye hilo.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga nyumba za Walimu katika Halmashauri ya Ikungi?

Supplementary Question 5

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tatizo lililopo Ikungi na Wilaya ya Mbogwe lipo. Je, ni lini sasa Serikali itawajengea walimu wa Wilaya ya Mbogwe nyumba ili na wao wapate pa kuishi? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nicodemas Maganga Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza awali, mkakati wa Serikali sasa hivi ni kutafuta fedha, kadri tunavyopata fedha maana yake tunajenga. Nimeainisha hapa kwamba siku hizi tunajenga Sekondari na kila Sekondari tunaweka nyumba za walimu three in one, yote hiyo ni mkakati wa kuondoa hii adha ya nyumba za walimu. Kwa hiyo. hata hapo Mbogwe nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge, Serikali tutaendelea kuleta fedha kwa kadri zitakapopatikana, kwa hiyo aondoe shaka kwenye hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.