Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 50 2022-04-13

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga nyumba za Walimu katika Halmashauri ya Ikungi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Tais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu Mbunge wa singida Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya mahitaji ya Nyumba za Walimu Nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya Ikungi.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Ikungi ina mahitaji ya nyumba 454 na nyumba zilizopo ni 172, ili kukabiliana na upungufu uliopo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya Ikungi imetenga Shilingi Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba nne za Walimu katika shule za Mandigu Kata ya Munga, Nali - Kata ya Siuyu, Mankumbi - Kata ya Kikio na Mau - Kata ya Ikungi.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu kwa Halmashauri ikiwemo na Halmashauri ya Ikungi kadri fedha zitakavyopatikana.