Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Fulo kupitia Nyambiti hadi Malya itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa TANROADS Mkoa wa Iringa walitii agizo la kwenda kuangalia barabara ya Mchepuko wa Mlima Kitonga, na tayari wameshafanya maandalizi ya awali. Je, Serikali inasemaje kuhusu kuanza usanifu na kuijenga barabara hiyo ya Mchepuko wa Mlima Kitonga ili wananchi waweze kupita kwa urahisi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyokiri kwamba tayari tumeshatoa maelekezo na baada ya kuipitia barabara sasa kinachofuata ni kuanza kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, suala hilo litafanyika kwa sababu ndiyo barabara itakayotuokoa ikitokea changamoto yoyote katika Mlima kitonga. Ahsante.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Fulo kupitia Nyambiti hadi Malya itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, Barabara hii ya Fulo kupitia Nyambiti mpaka Malya ni barabara ya muhimu sana kwenye uchumi wa Serengeti ya Kusini, na ni barabara ambayo Serikali imekuwa ikiahidi kuendelea kutafuta pesa, wakati huo Serikali ikitambua Jimbo la Sumve hatuna hata milimita moja ya lami.

Je, ni lini sasa seriously pesa hizi zitapatikana, mkafanya upembuzi yakinifu na kuanza kuijenga barabara hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, barabara yenye urefu wa kilometa 71 inayotokea Magu inapita Bukwimba – Nkalalo – Ngudu mpaka Hungumalwa nimekuwa nikiiombea kila mara ijengwe kwa kiwango cha lami na Serikali mlijibu kwamba sasa mmejipanga kuijenga katika bajeti hii.

Je, sasa ni lini ujenzi huo unaanza au inaendelea kupewa ahadi kama ambavyo imekuwa kawaida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kasalali Emmanuel Mageni, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nakubaliana naye, barabara hii bado haijafanyiwa usanifu ; na nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna barabara mbili tu ambazo zilikuwa bado hazijafanyiwa usanifu katika Mkoa wa mwanza ikiwepo hii. Tumeshamwagiza Meneja wa Mkoa aangalie kama kutatokea saving yeyote kwenye hela ya maendeleo, hii barabara tuanze. Tukuhakikishie barabara hii lazima itafanyiwa usanifu katika kipindi cha mwaka wa bajeti huu tunaokwenda na mpango wa sasa.

Mheshimiwa Spika, suala la pili, barabara ya Hungumalwa hadi Magu, Mheshimiwa Mbunge nishahidi, Waziri ameongea naye na tumeshaahidi. Tayari Meneja wa Mkoa ameelekezwa aitangaze kuianza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Fulo kupitia Nyambiti hadi Malya itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi ya swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Kiranjeranje – Nanjirinji mpaka Ruangwa imefanyiwa upembuzi wa kina na upembuzi yakinifu kwa lengo ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Wakati Wana-Nanjirinji tukisubiri lami, hali ya barabara hii si nzuri, hususan maeneo kutoka Mangaja – Nakiu – Nanjirinji mpaka Ruangwa, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutoa maelekezo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa wa Lindi ili wakakagua barabara hii na wafanye utaratibu wa dharura?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilifanyiwa usanifu wa awali, na mwaka huu tunakamilisha usanifu wa kina. Kwa hali aliyoelezea nataka tu nitumie fursa hii kumuagiza meneja wa TANROADS aende aiangalie hiyo barabara na kama kutakuwa na changamoto kubwa inayohitaji msaada wa Wizara basi tuweze kuwasiliana; lakini tunavyoongea leo aende aitembelee hiyo barabara ili aweze kurekebisha na wananchi waendelee na shughuli zao za kawaida. Ahsante.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Fulo kupitia Nyambiti hadi Malya itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona niulize swali la nyongeza. Pamoja na nia njema ya Serikali kupeleka miradi ya barabara za lami kwenye Jimbo la Kibamba hata hivyo pamekuwa na sintofahamu ya miradi hiyo kutobeba components za fidia zaidi ya migogoro na wananchi. Je, Serikali inasema nini juu ya jambo hilo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE: Mheshimiwa Spika, naomba nimwombe Mheshimiwa Issa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, aweze kuwasilisha swali kama swali kwa maana ya masuala ya fidia. Ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Fulo kupitia Nyambiti hadi Malya itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza swali, ni lini sasa barabara inayotoka Chang’ombe kupitia DUCE mpaka Mgulani mtamalizia, kwa sababu sasa hivi malori ni mengi sana ambayo yanapeleka vifaa viwandani na njia haipitiki sasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, labda tu nichukue nafasi hii kumuhimiza mkandarisi lakini pia na Meneja wa TANROADS kuhakikisha kwamba barabara hii inakamilishwa haraka. Mheshimiwa Mbunge kama kutakuwa na changamoto ya ziada naomba tuonane nae ili tuweze kutatua hiyo changamoto kama ipo kwa upande usimamizi ama kwa mkandarasi mwenyewe. Ahsante.