Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 135 2022-11-10

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Fulo kupitia Nyambiti hadi Malya itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kasalali Emmanuel Mageni, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuifanyia Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina barabara ya Fulo – Sumve – Nyambiti hadi Malya kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikitafuta fedha za Usanifu, Wizara kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), itaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili kuhakikisha kuwa inapitika vizuri majira yote. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya shilingi milioni 668.345 zimetengwa kwa ajili ya kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hiyo. Ahsante.