Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika,ahsante. Kwa mara ya pili ninaomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, Tarafa ya Ikuwo haina Mahakama ya Mwanzo, wananchi wanalazimika kusafiri zaidi ya kilimita 100 kwenda kupata huduma za kimahakama kitu ambacho kinawafanya wananchi wakate tamaa wasiendelee kufuatilia haki zao. Ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Mwanzo kwenye Tarafa ya Ikuwo ili wananchi wangu waweze kupata huduma hiyo. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika hali ya kawaida nimuombe Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane baada ya kikao hiki ili niweze kumpa mkakati ambao tumeuweka, kwa sababu katika kipindi hiki tuna miradi Sitini ambayo iko katika hatua mbalimbali na kwa sababu katika kipindi hiki tunayo miradi 60 ambayo ipo katia hatua mbalimbali na kwa sasa, kwa vile sina kumbukumbu sahihi hapa niwasiliane naye ili niweze kumsaidia kujua Mahakama yake inaenda kuanza lini ujenzi. (Makofi)

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 2

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa, Serikali inaendelea na ujenzi wa Mahakama za Wilaya na kule Wilayani Mkinga Mahakama yetu ya Wilaya iko tayari na imeanza kazi wiki iliyopita. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kukarabati zile Mahakama za Mwanzo ambazo ni chakavu sana. Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mhesimiwa Spika, ahsante sana, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu, Mbunge Viti Maalum kutokea Mkinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sasa hivi katika mpango wetu tunaoendelea nao, tunaendelea kukarabati na kujenga majengo mapya katika maeneo mbalimbali. Hivyo nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba majengo yaliyochakaa yataendelea katika utekelezaji wa mpango tulionao katika kipindi hiki tulicho nacho na kipindi kijacho kwa sababu mwisho wa mradi huu ni 2025 kuhakikisha kwamba huduma za Mahakama zote nchini katika ngazi mbalimbali tutakuwa tumezikamilsha. Ahsante.

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri sana ya Serikali yanayotia moyo, naomba naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Katika Kata ya Iguguno kuna Mahakama ya Mwanzo ya kisasa kabisa na ya kidigitali. Je, Serikali sasa haioni haja ya kuanza Mahakama ya Wilaya kwa muda katika Kata hii, kwani wanachi wanapa shida sana kwenda Wilaya ya Iramba kwenda kufuata Mahakama ya Mwanzo?

Swali la pili, iwapo Serikali itaridhia kutumia Mahakama hii; je, itakuwa tayari sasa kutumia mahabusu ya Singida Mjini badala ya kwenda Kiomboi kwani uhakika wa usafiri wa Singida Mjini ni rahisi na ni karibu zaidi? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kimsingi maoni yake yote tunayachukua na tunakwenda kuyafanyia kazi kuona Je, kuna uwezekano wa kuanza kutumia huduma zote hizi mbili ambazo Mheshimiwa Mbunge amependekeza. Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, wananchi wa Jimbo la Geita Vijijini wanalazima kufuata huduma za Mahakama ya Wilaya kilometa 60. Je, ni lini Wizara itakuwa tayari sasa kwenda kujenga Mahakama ya Wilaya kwenye Jimbo hilo?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sasa hivi tuko kwenye mkakati wa kuendelea na utekelezaji wa ujenzi wa Mahakama za Wilaya katika Wilaya 18. Ninapenda tu kumwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba ujezi wa jengo ambalo linahitajika katika Wilaya yake linaenda kuanza katika kipindi cha fedha kijacho kwa ajili ya kutekeleza mpango huu wa maboresho ya Mahakama nchini. Ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 5

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ni miaka minne sasa nikiendelea kutetea ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbulu. Kwa kuwa, sasa mahakama ya Wilaya inapitiwa na ujenzi wa barabara ya lami. Je, ni lini Serikali itatekeleza azma yake ya ujenzi wa Mahakama yetu hiyo?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kutoka Mbulu. Wilaya ya Mbulu ni miongoni mwa Wilaya ambazo ziko kwenye mkakati wa kujengewa Mahakama kwa kipindi hiki cha fedha cha 2022/2023. Kwa hiyo taratibu za kupata Mkandarasi kwa ajili ya zoezi hilo zinaendelea. Ahsante.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 6

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Uyui iko kwenye chumba kidogo sana tulichopewa na Ofisi ya DC.

Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Uyui? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kutoka Uyui kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika jibu la msingi, ni kwamba sasa hivi Mahakama ya Tanzania imeendelea katika shughuli za ujenzi wa Mahakama mbali mbali hapa nchini. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge, tuwasiliane baada ya kipindi hiki ili niweze kumuweka katika kumbukumbu zilizo sahihi juu ya lini tunaenda kuanza ujenzi katika eneo lake. Ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 7

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, napenda kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kujenga Mahakama mpya nzuri ya Wilaya ya Kilombero. Swali, je, ni lini Mahakama ile itazinduliwa katika Kata ya Kibaoni pale ili wananchi wawenze kupata huduma za Mahakama Mpya?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kutoka Kilombero. Ni kwamba wakati wowote atajulishwa utaratibu wa uzinduzi wa ile Mahakama kwa sababu haijaisha muda mrefu sana. Sasa hivi tunaharakisha uzinduzi wa Mahakama zote ambazo zimekamilika hapa nchini kwa ajili ya kuzizindua. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuzijenga na kukarabati Mahakama za mwanzo za Nkwaranga na West Meru, kama ilivyoahidi mwaka wa fedha uliopita 2021?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimuombe Mheshimiwa Pallangyo tuwasiliane ili niweze kumpa mkakati halisi, lakini mpango kazi wote umeshakamilika katika kukarabati na kujenga majengo mapya ya maeneo ambayo hayana mahakama. Kinachokosekana hapa ni kumbukumbu sahihi tu, kwa sababu swali linakuwa limekuja kwa sasa hivi. Ahsante.