Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 134 2022-11-10

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya katika Halmashauri ya Mkalama?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Tanzania inaendelea kutekeleza mpango wake wa kuhakikisha kuwa kila Wilaya inakuwa na jengo la Mahakama. Aidha kwa sasa miradi inayoendelea ni ujenzi wa majengo ya Mahakama za Wilaya 18. Ujenzi wa Jengo la Mahakama ya Wilaya ya Mkalama umepangwa kufanyika katika mwaka huu wa fedha 2022/2023. Kwa sasa taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi zinaendelea. Ahsante. (Makofi)