Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanzisha vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza pia nikushukuru kwa kunipa nafasi kwamba swali hili lirudiwe leo kwa mara ya tatu.

Kwa kuwa, Kata ya Bombo lijenga Ofisi yake ya Kata na ikaweka nafasi ya Polisi pamoja na chumba cha mahabusu. Kwa kutambua kwamba hizi sehemu zote ulizoongelea ziko tambarare na hawa wakazi wa Kata Tisa zote wako milimani ambako usafiri ni shida sana. Je, Serikali haioni ianzishe kituo mnaita Police post ili angalau katika Kata hii ya Bombo kiwepo kusaidia wananchi walioko huko milimani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kuwapongeza wananchi wa eneo hilo kwa kujenga jengo la utawala ngazi ya Kata na kutenga eneo kwa ajili ya huduma za Kipolisi. Nitumie nafasi hii kuelekeza Jeshi la Polisi hususani Mkoa wa Kilimanjaro kutembelea eneo hilo kuona kama ujenzi ule unakidhi kuwa Kituo cha Polisi basi huduma za kipolisi zianze kutolewa kwenye eneo hilo. Nashukuru. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanzisha vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi hii. Kwa kuwa, Tarafa ya Gonja na Tarafa ya Mambavunta ni Tarafa ambazo ziko kwenye milima mikubwa sana na hiki Kituo cha Polisi cha Gonja wanapata shida sana kuwafikia wananchi kule milimani.

Je, Serikali haioni umuhimu mkubwa sana wa kupeleka gari lenye uhakika kwenye Kituo cha Afya cha Gonja ili waweze kuwahudumia wananchi wangu walioko kwenye Tarafa zile ambazo ni ngumu sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango Malacela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hii Kata aliyoitaja ya Gonja iko milimani na ni changamoto kubwa kutoka maeneo ya tambarare kuwahudumia wanachi kule milimani. Tunatambua umuhimu wa gari tumeeleza hapa juzi hivi sasa tulipata magari 78, na tumeweza Mkoa wa Kilimanjaro kuupatia magari mawili, ni ahadi yetu kwa Mheshimiwa Mbunge kulingana na changamoto ya usafiri wa eneo hilo tutakapo pata magari eneo hilo litafikiriwa na kupewa kipaumbele. Nashukuru. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanzisha vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Tarafa ya Kalenga katika Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli sasa hivi mwelekeo tumekwenda mpaka ngazi ya Kata tumepeleka maofisa wetu wakaguzi na wakaguzi wasidizi kwa ajili ya kusomamia Shughuli za polisi. Sasa iwapo Kata ya Kalenga haina tutaipa kipaumbele ili kata hii iweze kingatiwa hatimaye vijana wetu waweze kufanya kazi kwenye mazingira stahiki ya kutoa huduma za usalama wa raia na mali zao. Ahsante.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanzisha vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Supplementary Question 4

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Jimbo la Tunduru Kusini lina Tarafa Tatu. Tarafa ya Namasakata haina Kituo cha Polisi na ndiyo iliyopo mpakani na Msumbiji.

Je, ni lini Serikali itapeleka Kituo cha Polisi katika Tarafa hii ya Namasakata?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mpakate, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ninamshauri Mheshimiwa Mbunge ikiwa Tarafa hii haina kituo cha kwanza tutafute ardhi. Ardhi ikishapatikana tuipime tukabidhi Jeshi la Polisi hatimaye tuweze kuingiza eneo hilo kwenye mpango wetu wa ujenzi wa Kituo cha Polisi. Kwa vile anasema kiko mpakani inahitaji kwa kweli ulinzi eneo hilo na tutakupatia kipaumbele iwapo upatikanaji wa ardhi utatekelezwa mapema. (Makofi)