Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 133 2022-11-10

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanzisha vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge Wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na vituo vya Polisi katika maeneo mbalimbali nchini kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi. Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta hazina vituo vya polisi wala maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi na Nyumba za Makazi ya Askari. Wananchi wa Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta hupata huduma za polisi toka vituo vya polisi vya Same mjini na Gonja, na vituo vidogo vya polisi vya Kihurio na Ndungu.

Mheshimiwa Spika, ni ushauri wangu kwa Mheshimiwa Mbunge kushirikisha Halmashauri ya Wilaya ya Same kutenga maeneo katika tarafa za Mamba na Gonja kwa ajili ya kujenga kituo cha Polisi pamoja na Nyumba za Makazi ya Askari, ili Serikali iweze kuweka kwenye mpango wake wa Bajeti kwa ajili ya utekelezaji. Nashukuru. (Makofi)